Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Fyatu kushinda urahis wa mafyatu kimiujiza

Najua. Kaya yetu inafanya uchakachuaji, sorry, uchaguzi mwaka huu. Sambamba, nasi mafyatu tutafanya uchaguzi si uchakachuaji wa rahis wa mafyatu Mheshimiwa, Daktari, Profesa, ustaadh, Al haj, Muadhamu, Mtakatifu, Muona Mbali Fyatu Mfyatuzi. Hivyo, ili kujihakikishia ushindi wa kishindo na wa miujiza, nimeweka mikakati ifuatayo:

Mosi, nitahakikisha nashinda hata kwa bao la kisigino watake wasitake. Mwenye wivu si ajinyongelee mbali.

Pili, nitatoa ahadi kama sina akili nzuri. Lazima niwaaminishe mafyatu kuwa mimi ndiye ninafaa hata kama sifai. Lazima wajue kuwa bila mimi, watayumba na kuteseka sana.

Tatu, nitahakikisha wapingaji wenye kuonyesha ushawishi wanafunguliwa kesi za wizi wa kuku au za kubambikizwa. Pia, nitawaambia na kuwaaminisha mafyatu kuwa wanapaswa kuwaogopa wapingaji kama ukoma. Hii ni kutokana na ukweli kuwa wanatumiwa na ‘maadui’ wa mafyatu toka ughaibuni wanaotaka kuharibu amani, ulaji, na utulivu wetu.

Nne, nitaamuru migambo yetu kuwasweka ndani wote wanaoonyesha kutishia ushindi wangu.

Hapa, lazima kusiwe na huruma, haki za mafyatu wala nini, bali kufanya kweli kwa kuteka, kutembeza kipigo, na ikibidi kuweka ndani bila kutoa maelezo wala kufuata sheria za mafyatu.

Tano, nimehakikisha mafyatu wananipitisha, siyo kunichagua kama kanuni za katiba ya mafyatu inavyotaka kwenye kura za mchujo na uchaguzi wa ndani ya chata letu tukufu. Mafyatu wasenzi kweli.

Si wapo waliotaka eti nipambanishwe na wanachama wengine wa Chama Cha Mafyatu (CcM) ili kupata mgombea anayekubalika. Niliwazuia kutenda dhambi hii ya kunipambanisha mie mtukufu na watukutu katika chama chetu. Nani hajui kuwa mie napendwa na kukubalika? Anayebisha aulize miti, wadudu, hata wanyama. Mie nakubalika bwana. Anayeendelea kushuku hili, ajiulize ni kwa nini nasifiwa kwa kila jambo hata lisilopaswa.

Sita, nitahakikisha wakati wa kampeni hakuna kuwapa nafasi wapingaji wangu kufanya kampeni. Tena nitumie fursa hii kutoa angalizo na onyo.

Yeyote atakayeshirikiana na wapingaji wangu ajue. Atakipata cha moto. Wao kama nani wafanye kampeni sawa nami wakati wanajua wazi mshindi ni mimi?

Nani aruhusu wapingaji wavuruge amani na utulivu wa mafyatu? Mafyatu hawajui kuwa niliapishwa kulinda ulaji na si wao? Je, huu siyo muujiza unaolenga kuleta amani na mshikamano chamani?

Saba, kwa mjibu wa katiba ya CcM, mwenyekiti ana turufu ya kuteua wasimamizi wa wilaya na mikoa kama ilivyo kwa lisiri kali.

Hivyo, nimewaamuru watendaji wangu wote kuhakikisha wanatumia mamlaka niliyowapa kuzuia upuuzi unaoitwa mikutano ya hadhara. Hii si mikutano ya hadhara, bali ya madhara. Nani anapenda madhara wakati huu wa kusaka ulaji wa dezo, tena mnene?

Atakayekaidi agizo hili ambalo, kifyatu, ni sheria, natengulia mbali uteuzi wake tuone kama atakula mafi yake nyambaff.

Nane, nitaamuru vyombo vya umbea vyote vya kifyatu kutangaza sera zangu pekee, huku vikihakikisha vinawabana na kuwakandia kwa kuwanyima fursa ya kutangaza utopolo wao wapingaji.

Atakayekaidi na kutangaza ujinga wa wapingaji, ama nitamfungia au kumnyima matangazo ya biashara, au kufutilia mbali chombo chake nione kama atakula jeuri yake.

Tisa, nitanunua na kupandikiza vyama pandikizi ili ‘vishindane’ nami ili kuhalalisha miujiza yangu katika kushinda uchakachuaji, sorry, uchaguzi kwa kishindo na miujiza vinafanikiwa.

Viongozi wa vyama hivi lazima niwapige njuluku walainike na kujifanya wananipinga wakati game letu ni moja au siyo? Kwa usawa huu, bila kuja na mikakati kama hii, unaweza kuadhirika bure mzee mzima ukatupwa nje ya ulaji na kuchekwa hata kufunguliwa mashtaka kwa makosa ambayo nimeshafyatua.

Nawajua mafyatu. Hawana akili nzuri wala dogo.

Kumi, napanga uchakachuaji, sorry, uchaguzi uwe wa amani na utulivu.

Hivyo, ili kuhakikisha hivi vinafanyika, migambo watatembeza kipigo kwa yeyote anayetaka kutishia amani na utulivu wa ulaji wangu na wapambe wangu.

Kumi na moja, ili kuwaweka sawa mafyatu, nitaanza kuhubiri amani kwa kuwatishia na migogoro na vita vinavyoendelea kwenye kaya za mafyatu jirani.

Lazima wajue kuwa bila mimi kuukwaa urahis, mafyatu wote watakabiliwa vita na matatizo makubwa.

Kufanikisha hili, nitaamuru runinga zote za mafyatu kuonyesha madhara ya migogoro na vita husika. Kwa niwajuavyo mafyatu, bila kuwatisha, wanaweza kunitisha hata kutishia ulaji wangu mtukufu.

Kumi na mbili, kuanzia sasa hadi uchakachuaji, sorry, uchaguzi, nitaanza kumwaga misaada kila mahali ili mafyatu wanichague.

Najua. Kumi na tatu, nitahakikisha mwanangu mwenyewe ndiye atakayesimamia wizara ya mafyatu inayosimamia mambo ya uchakachuaji ili tusije kupigwa bao la kisigino na wabaya wangu waliojazana kwenye chama chetu.

Kumi na nne, nitaanza vita na mataifa yanayojifanya vijogoo na kutaka kutufundisha demokrasia na haki za mafyatu kana kwamba mafyatu wangu ni wao.

Du! Ndoto nyingine zikichanganyika na bangi ni balaa! Kumbe naota urahis siyo urais!