Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Mwinyi ataja maeneo matatu Zanzibar kushirikiana na Ujerumani

Unguja. Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi ameendelea na ziara yake nchini Ujerumani leo Jumatatu Juni 19, 2023 amekutana  na Katibu wa Bunge Upande wa Wizara ya Ushirikiano wa kiuchuni na Maendeleo nchini Ujerumani Dk Barbel Kofler.

Katika mazungumzo yao yalijikita zaidi kuimarisha uhusiano uliopo baina ya Tanzania hususani Zanzibar kwa upande mmoja na Ujerumani.

Rais Mwinyi amemueleza Dk Kofler maeneo matatu ambayo Zanzibar ingependa zaidi kushirikiana na Ujerumani ikiwemo nchi hiyo kusaidia miradi ya maji, michezo na afya.

Pia namna ya kujenga misingi ya kuimarisha usimamizi  wa matumizi ya fedha za miradi.

Naye, Dk Kofler amempongeza Rais Mwinyi kwa kuwa na mawaziri sita wanawake ndani ya Serikali anayoiongoza hatua inayodhihirisha kuwaongezea uwezo wanawake.

Katika hoja hiyo, Rais Mwinyi amemuhakikishia Dk Kofler kwamba viongozi wanawake aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali wanafanya kazi nzuri na huenda akawapa nafasi wengi zaidi.

Rais Mwinyi yupo nchini Ujerumani pamoja na mambo mengine, alihudhuria ufunguzi wa mashindano ya Olimpiki maalumu ambapo Tanzania inawakilishwa na vijana 20.