Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Haya hapa majina manusura Kariakoo waliopokelewa Muhimbili

Muktasari:

  • Muhimbili ilitoa majina hayo jana usiku Novemba 16, 2024

Dar es Salaam. Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), imetoa orodha ya majina 40 ya manusura wa ajali ya jengo la ghorofa kuporomoka Kariakoo waliopelekwa hospitalini hapo kwa matibabu.

Jengo hilo lililoporomoka jana Jumamosi Novemba 16, 2024 asubuhi huku jitihada mbalimbali za uokozi zikiendelea kufanywa kwa uratibu wa Serikali.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha, imesema hadi ilipotimu saa 11 jioni jana, manusura 35 waliruhusiwa kurudi nyumbani.

Hata hivyo, leo asubuhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema mpaka jana usiku manusura waliookolewa walikuwa 70 huku waliofariki dunia wakiwa wane.