Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ghorofa laporomoka Dar, watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha

Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha baada ya jengo moja la ghorofa lililopo Kariakoo Mtaa wa Congo na Mchikichi jijini Dar es Salaam kuporomoka.

Jengo hilo linaelezwa kuporomoka mapema leo Jumamosi Novemba 16, 2024. Taarifa za awali kutoka kwa mashuhuda, zinaeleza kuwa ndani ya jengo hilo la kibiashara, kulikuwa na watu kadhaa waliokuwa wakifanya ununuzi katika maduka ya jengo hilo.

Polisi kwa kushirikiana na wananchi wanaendelea na juhudi za uokoaji.
Zaidi aendelea kuifuatilia Mwananchi Digital.