Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Uokozi jengo lililoporomoka Kariakoo waingia siku ya pili

Uokoaji ukiwa unaendelea Kariakoo

Muktasari:

  • Ni asubuhi ya siku ya pili tangu jengo hilo lililoporomoka jana Novemba 16, 2024, shughuli mbalimbali za uokozi zinaendelea.

Dar es Salaam. Shughuli za uokoaji zinaendelea asubuhi hii katika jengo la ghorofa lililoanguka Kariakoo jijini Dar es Salaam zikiwa zinaingia siku ya pili tangu tukio hilo litokee.

Asubuhi ya leo Jumapili, Novemba 17, 2024 mtu mwingine ameokolewa, wakati akitolewa kuna mtu amemtambua kwa kumuita jina moja la Michael.

Jengo hilo lililoporomoka jana Jumamosi Novemba 16, 2024 asubuhi, mpaka sasa jitihada mbalimbali za uokozi zinafanyika.

Hata hivyo, mpaka jana usiku, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), ilitoa orodha ya majina 40 ya manusura wa ajali ya hiyo waliopelekwa hospitalini hapo kwa matibabu.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha, inasema hadi ilipotimu saa 11 jioni , manusura 35 waliruhusiwa kurudi nyumbani.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kwa taarifa aliyoitoa asubuhi ya leo ni kuwa manusura 70 hadi jana waliokolewa huku watu wane wakifariki dunia kutokana na ajali hiyo.


Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi