Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Baba adaiwa kumuua mwanaye

Muktasari:

  • Jeshi la polisi mkoani kilimanjaro  linamshikilia mkazi wa kijiji cha Challa wilayani Rombo, John Kavishe (77) kwa tuhuma za  kumuua mwanaye,   Amedeus  (31) kwa kumkata na panga shingoni wakati akisuluhisha ugomvi wa kifamilia.

Rombo. Jeshi la polisi mkoani kilimanjaro  linamshikilia mkazi wa kijiji cha Challa wilayani Rombo, John Kavishe (77) kwa tuhuma za  kumuua mwanaye,   Amedeus  (31) kwa kumkata na panga shingoni wakati akisuluhisha ugomvi wa kifamilia.

Kamanda wa polisi mkoani humo, Simon Maigwa amesema  tukio hilo limetokea  Julai 10, 2021.

"Marehemu alikuwa na ugomvi na mke wake ndipo baba mzazi alipokwenda kusuluhisha  kitendo hicho kilimchukiza marehemu akaanza kumtukana baba yake ambaye alipandwa na hasira na  kuchukua panga na kumkata mwanaye shingoni," amesema Kamanda Maigwa.

Amebainisha kuwa mwili  wa kijana huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Ngoyoni kilichopo wilayani Rombo.