Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ushauri mgumu kwa Liverpool sakata la Salah

Muktasari:

  • Salah alimaliza akiwa kinara katika chati ya kufumania nyavu ya Ligi Kuu England msimu uliopita akifunga mabao 29.

Kiungo za zamani wa Liverpool, Dietmar Hammann ameitaka klabu hiyo kuachana haraka na mshambuliaji wa Misri, Mohamed Salah kwa vile mchezaji huyo hajaonyesha heshima kwa timu.

Hammann ametoa kauli hiyo ikiwa ni muendelezo wa mastaa mbalimbali wa zamani wa soka wa klabu hiyo na wengineo kutoa maoni yao juu ya kitendo cha Salah kutoa tuhuma hadharani kuwa timu hiyo haimtendei haki baada ya kuwekwa benchi katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Leeds United wikiendi iliyopita.

Hammann ambaye amewahi pia kuitumikia timu ya Taifa ya Ujerumani, amesema kuwa Salah ameonyesha ubinafsi wa hali ya juu hivyo hafai kuendelea kuitumikia Liverpool.

"Sidhani kama tutamuona tena katika jezi ya Liverpool. Anaenda katika Kombe la Afrika muda mfupi ujao na kwa maoni yangu, muda wake ndani yaLiverpool umeisha.

"Amecheza ovyo kwa miezi 10, 11. Kulikuwa na fursa ya kutosha kumuweka benchi. Hadi wiki mbili zilizopita, kocha alimpanga na kumpa imani yake. Baada ya hapo hakukuwa na njia nyingine.

"Liverpool ipo katika presha kubwa. Haiendi vizuri na baadaye Salah anaweza kufikiria hakuna kilicho bora baada ya mechi ambayo umeruhusu bao la kusawazisha katika dakika ya mwisho na kisha kusimama na kulalamika kuhusu suala lake binafsi," amesema Hammann.

Msuguano kati ya Salah na Slot umekuwa ukiendelea kwa miezi kadhaa lakini sasa umelipuka hadharani.

Slot alichukua uamuzi wa kijasiri kumweka benchi mchezaji huyo raia wa Misri anayelipwa pesa nyingi zaidi klabuni hapo.

Hatua hiyo ililenga kuzua hisia, lakini badala yake, ilisababisha mkutano na vyombo vya habari ambapo mshambuliaji huyo alilalamikia kutowekwa wazi juu ya mustakabali wake na jukumu lake ndani ya kikosi.

Hamann amekasirisha haswa na nyakati ambayo Salah ametoa malalamiko hayo. Anaamini kwamba kwa kutanguliza malalamiko ya mkataba wake juu ya kukatishwa tamaa huku timu ikiwa imetoka sare, Salah huyo amevuka mstari ambao hauwezi kuvuka.

"Ikiwa una tatizo, nenda kwa kocha. Sina uelewa kwa hilo. Yeye ni mmoja wa wachezaji wakubwa wa Liverpool katika historia. Hakuna swali, lakini ameharibu mengi na hii, akiweka masilahi yake juu ya yale ya kilabu," amesema Hammann.