Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Shabiki amvamia Ronaldo uwanjani

Muktasari:

  • Mshambuliaji nyota wa Juventus Cristiano Ronaldo amevamiwa na shabiki uwanjani wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Italia.

Rome, Italia. Cristiano Ronaldo amevamiwa na shabiki uwanjani katika mchezo ambao Juventus ilishinda mabao 3-0 dhidi ya Sassuolo.

Shabiki huyo alimvamia mchezaji huyo baada ya kuvamia uwanja na kwenda kumkumbatia wakati mchezo huo ukiendelea.

Tukio hilo lilitokea kipindi cha pili, baada ya shabiki huyo kuonyesha furaha yake kutokana na kiwango bora cha Juventus.

Ronaldo alifunga bao moja katika mchezo na mengine yalifungwa na Sami Khedira na Emre Can.

Ronaldo aliyejiunga na Juventus akitokea Real Madrid katika usajili wa majira ya kiangazi msimu uliopita, amefunga mabao 20.