Dk Mwinyi ateua majaji wanne, yumo Raya
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi
Muktasari:
- Baada ya uteuzi huo, Mahakama Kuu ya Zanzibar imefikisha Majaji wa Mahakama Kuu 18
Unguja. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amewateua majaji wanne wa Mahakama Kuu Zanzibar akiwemo Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Raya Issa Msellem.
Pia amemteua Dk Mahadhi Juma Maalim kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Zanzibar.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mansura Mosi Kassim, uteuzi huo umeanza leo Julai 15, 2026.
Taarifa hiyo imewataja majaji wengine walioteuliwa ni Valentine Andrew Katema ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa mrajisi wa Mahakama Kuu Zanzibar.
Mwingine ni Khamis Ali Simai ambaye kabla ya uteuzi alikuwa Hakimu wa Mkoa.
Baada ya uteuzi huo, Mahakama Kuu ya Zanzibar imefikisha majaji 18.