Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Makocha walio kwenye hatari ya kutimuliwa Ligi Kuu England

Muktasari:

  • Arne Slot ndiye jina kubwa zaidi, baada ya kuiongoza Liverpool kwenye msimu mgumu wa kutetea Ubingwa.

Ikiwa zimesalia mechi 15 pekee kumaliza msimu wa Ligi Kuu England 2025/26, baadhi ya makocha huenda wasiuone mwisho wa kampeni hii. Miongoni mwao ni Thomas Frank, Arne Slot na Oliver Glasner, ambao wapo katika presha kubwa kutokana na matokeo yasiyoridhisha.

Msimu huu tayari umeshuhudia vichwa kadhaa vikikatwa. Nuno Espírito Santo alikuwa wa kwanza kuondolewa Septemba baada ya kufukuzwa na Nottingham Forest.

Baadaye Graham Potter, Ange Postecoglou na Vítor Pereira nao waliondolewa kadri nusu ya kwanza ya msimu ilivyokuwa ikiendelea.

Hata vigogo wa ligi hawakusita kuchukua hatua kali. Rúben Amorim na Enzo Maresca waliondolewa na Manchester United na Chelsea mapema mwezi huu, ndani ya siku chache tofauti.

Kwa zaidi ya theluthi moja ya msimu bado kucheza, uwezekano wa kuona makocha wengine wakiondolewa bado upo. Hawa ndio walioko katika hali tofauti za hatari:


WAKO SALAMA

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta anaiongoza ligi na hana hofu ya kuondolewa. Pep Guardiola anaendelea kuwa na heshima kubwa Manchester City, huku Unai Emery akifanya kazi nzuri Aston Villa.

Kwa Sunderland, Régis Le Bris ameonyesha ubora mkubwa katika msimu wake wa kwanza, hivyo mabadiliko ya benchi la ufundi yanaonekana kuwa ndoto.

Keith Andrews amewanyamazisha waliomtilia shaka kabla ya msimu kuanza kwa kazi nzuri Brentford. Vilevile, Michael Carrick wa Man United na Liam Rosenior wa Chelsea wameajiriwa hivi karibuni, hivyo wako salama kwa sasa.

Kwa timu za katikati ya msimamo, Marco Silva ameifikisha Fulham nafasi ya saba, huku David Moyes, Fabian Hürzeler na Andoni Iraola wakifanya kazi za kuridhisha, hali inayowapa uhakika wa kuendelea kwa sasa.


WAKO HATARINI

Baada ya walio salama, kuna kundi la makocha wanaohitaji kuwa waangalifu. Arne Slot ndiye jina kubwa zaidi, baada ya kuiongoza Liverpool kwenye msimu mgumu wa kutetea Ubingwa.

Kipigo cha dakika za mwisho dhidi ya Bournemouth kimeongeza presha kwake. Ingawa bado hayuko katika hatari ya kuondolewa mara moja, anahitaji haraka mwendelezo wa matokeo chanya.

Kocha wa Newcastle Eddie Howe pia yupo katika hali kama hiyo. Licha ya juhudi zake, wamiliki wa klabu wanatarajia kuona timu ikifuzu Ligi ya Mabingwa, jambo ambalo linaonekana kuwa gumu kwani hadi sasa Newcastle inashika nafasi ya tisa kwa pointi 33.

Daniel Farke wa Leeds amefaulu kuiondoa timu yake kwenye hali ngumu ya kushuka daraja, lakini msururu mwingine wa matokeo mabaya unaweza kumuweka pabaya. Sean Dyche naye yupo kwenye presha ndogo, huku Nottingham Forest wakiwa pointi tano tu juu ya eneo la kushuka daraja.

Kwa upande wa Nuno Espírito Santo, Rob Edwards na Scott Parker, kwa sasa hawapo kwenye hatari ya haraka, lakini mfululizo wa vipigo unaweza kubadili hali hiyo.


WAKO KWENYE HATARI KUBWA

Katika kundi la presha kubwa zaidi, jina la Thomas Frank linajitokeza wazi. Kocha huyo raia wa Denmark alichukua mikoba Tottenham majira ya kiangazi, lakini matokeo yamekuwa mabaya.

Spurs wapo nafasi ya 14, wakiwa na tofauti ya pointi nane juu ya eneo la kushuka daraja. Aidha, mashabiki wameanza kumpotezea imani, hali inayoweza kumnyanyua kwenye kiti chake endapo mambo hayatabadilika haraka.

Kwa upande wa Oliver Glasner, kocha wa Crystal Palace, hali nayo si shwari. Licha ya dalili kuwa huenda akaondoka mwishoni mwa msimu, inawezekana akaondolewa mapema. Kocha huyo amekuwa akiwakosoa viongozi wa klabu kufuatia kumuuza beki, Marc Guéhi, huku Palace wakikosa ushindi wa ligi kwa karibu miezi miwili.