Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mbeto asisitiza Tanzania kuendelea kuheshimu taasisi za kiraia, dini

Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis.

Muktasari:

  • Mbeto ameyataka makundi ya kisiasa, kidini na kijamii kutambua Serikali ya Tanzania tangu iundwe, haina dini na katika nyakati zote iliweka bayana msimamo wake kitaifa na kimataifa, haitajiegemeza katika dini

Dar es Salaam. Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeyaahidi makundi huru ya kijamii na madhehebu ya dini, kupokea ushauri na maoni huku ikiyataka kutambua Serikali ya Tanzania haina dini.

Pia, CCM imeyaasa makundi  hayo ikitaka yajue mantiki ya utawala wa sheria ni  utamaduni wa  kutatua hoja za kisheria;  kwa  mujibu wa sheria mahakamani  si kuicharaza bakora hoja  au kuipiga rungu.

Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati Maalumu  ya NEC  Idara  ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis  Mbeto  Khamis,  alipozungumza na waandishi wa habari  wakati  akituma salaam za Pasaka  kwa Wakristo wote duniani  kisiwani Unguja.

Mbeto amesema  makundi  hayo , yasilishinikize  Jeshi la Polisi kibabe na  vitisho  badala yake, watumie busara ya kutii sheria bila shuruti  wala chagizo .

Amesema ikiwa makundi hayo yataamua kila moja liseme kivyake au kuandamana bila kibali cha polisi, huku baadhi yao wakivua nguo na kutembea utupu, huko pia ni kwenda kinyume na sheria za nchi hivyo  watakamatwa.

"Kwa muda mrefu makundi hayo yamekuwa kimya hata pale baadhi ya wanasiasa wa upinzani  walipotoa matamshi ya kuogopwa.

“Ni matamshi mfululizo yalioambatana na vitisho kinyume na sheria. Jumuiya hizo zingetosha kuwaonya viongozi hao kwa kuwaelimisha, hivyo   wafanyavyo sivyo, "amesema Mbeto.

Katibu huyo mwenezi huyo, amesema kumeanza kusikika sauti za makundi hayo yakitaka pPolisi kumwachia   huru Mwenyekiti wa Chadema , Tundu  Lussu kutokana na  kesi inayomkabili mahakamani.

Mbeto ameyataka makundi hayo ya kisiasa, kidini na kijamii kutambua Serikali ya Tanzania tangu iundwe, haina dini na katika nyakati zote iliweka bayana msimamo wake kitaifa na kimataifa,   haitajiegemeza katika dini.

“Nchi yetu inafuata utawala wa sheria. Endapo kila mwanasiasa atakapokiuka sheria   yatoke  mashinikizo kwa  dhehebu  lake  haitaleta maana. Waumini wa dini moja wafuasi wake walikaa zaidi ya miaka kumi  mahabusu  hayakutokea madhehebu  yao kushinikiza, "amesema Mbeto.

Aidha Mbeto, amesema ikiwa  kiongozi wa kisiasa atakuwa wa Dhehebu la Wasabato, Waanglikana, Ethnaasheeria , Suni, Ismailia au Mkatoliki anayekabiliwa na kesi  mahakamani ,  viongozi wa madhehebu hayo  wakishinikiza  aachiwe mara moja  kutazuka utata na tafran  isiokuwepo.

"Joseph Kasela Bantu, Christopher Kassanga Tumbo,Modestus Choga na James Mapalala  walikaa vizuizini  katika  Serikali ya Mwalimu Julius  Nyerere . Viongozi wa dhehebu la kikatoliki waliheshimu uamuzi  wa Serikali . Utawala wa  Rais mstaafu Jakaya Kikwete ,  masheikh wa Kiislamu  walitupwa jela lakini  madhehebu yao zilitii  sheria,”amesema.

Pia, Mbeto  ametoa mfano mwingine, akimtaja Mchungaji Christopher  Mtikila ambaye alikuwa kiongozi wa chama  cha DP,  amekamatwa mara nyingi na hadi akafungwa jela, viongozi  wa dhehebu  lake hawakuzua mijadala yenye jazba .

"Tumemuona mwenyekiti mstaafu wa Chadema Freeman Mbowe  ni Mlutheri. Ameshitakiwa kwa tuhuma ya kesi ya ugaidi katika utawala wa marehemu  Rais Dk  John Magufuli. Amekaa mahabusu akatolewa na Serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan bila  shinikizo  lolote,”amesema Mbeto.

Katibu huyo mwenezi,  pia  ametoa mfano wa kesi ya uhaini ya wanasiasa  18 wa Chama cha CUF  katika utawala wa Rais mstaafu  Dk  Salmim Amour , watuhumiwa wote wakiwa   waislamu,  waliiachiwa huru katika utawala  wa Rais  mstaafu Dk Amani Abeid  Karume.

"Katika kesi ya uhaini ambayo kiongozi wake, Pius Lugangira na wenzake,  walifungwa jela maisha katika  utawala wa mwalimu Nyerere.   Wakaachiwa huru Awamu ya Pili ya Rais marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi bila  hekaheka  zozote, " amefafanua Mbeto.

Hata hivyo,  mwalimu  Nyerere aliwahi kukataa ombi la Kiongozi wa  dhehebu  la Orthodox  wa  Cyprus,  Askofu Makarios la  kutaka amwachie huru  mfanyabishara mmoja  aliyeleta kiburi na jeuri hadi  pale Nyerere  alipojiridhisha.