Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Foleni yawatesa madereva bandarini Dar

Muktasari:

Madereva wa malori walia na foleni ya bandarini, wadai wanakaa hadi siku tatu kusubiri kuingia


Dar es Salaam. Madereva wa malori yanayopandisha na kushusha mizigo katika bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania wamelalamikia foleni iliyokithiri katika kazi hiyo.

Madereva hao wameeleza kuwa kutokana na foleni hiyo wanalazimika kukaa hadi siku tatu kusubiri kuingia bandarini.

MCL Digital imefika katika eneo hilo leo Alhamisi Septemba 5, 2019 na kukuta msururu wa malori kutoka eneo la Uhasibu hadi bandarini ikiwa ni umbali wa  kilomita nne huku madereva wakiwa wamekata tamaa.

Akizungumzia hilo Nahad Kimela ambaye ni dereva amesema ana siku ya  tatu yupo kwenye foleni hiyo na hana matumaini ya kuingia ndani siku ya leo.

“Kwa kweli tunashindwa kuelewa hii foleni chanzo ni nini, siku hizi imekuwa kawaida, kinachotupa wakati mgumu msururu mrefu hata haijulikani nani anapakia nani anashusha,” amesema

Kilio kama hicho kimetolewa na Hemed Juma aliyeeleza kuwa yupo kwenye foleni hiyo tangu asubuhi ya jana.

“Tunapata wakati mgumu niko hapa tangu jana na hii sasa imekuwa kawaida, wala hakuna taarifa yoyote kwamba kuna kitu kuna shida hatuelewi shida nini kama ni utendaji au system,” amesema

Jitihada za kupata uongozi wa bandari ili kuelezea chanzo cha foleni hizo zinaendelea baada ya leo kukwama kupatikana.