Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Saba wafariki dunia ajali ya ambulance na toyo

Mafinga. Watu saba wamefariki dunia na wengine 15 kujeruhiwa katika ajali ya gari la kubeba wagonjwa (ambulance) kugongana na toyo katika eneo la Luganga, lililopo katika Halmashauri ya Mji Mafinga, Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa.

Akizungumza baada ya kutembelea majeruhi wa ajali hiyo leo Jumamosi, Aprili 19, 2025, Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dk Linda Salekwa, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Amesema kuwa taarifa zinaonyesha watu hao walikuwa wanakwenda shambani kufanya kazi, ndipo gari hilo likagongana na toyo hiyo na kusababisha watu hao kufariki dunia na wengine kujeruhiwa.


Endelea kufuatilia Mwananchi.