Mufti: Idd El Fitri kesho

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir
Muktasari:
- Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limetangaza kuandama kwa mwezi leo Jumapili Machi 30, 2025 hivyo swala ya Idd El Fitri itafanyika kesho Machi 31, 2025.
Dar es Salaam. Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limetangaza kuandama kwa mwezi leo Jumapili Machi 30, 2025 hivyo swala ya Idd El Fitri itafanyika kesho Machi 31, 2025.
Taarifa iliyotolewa na Bakwata katika mitandao ya kijamii leo Machi 31, 2025 imeeleza:
“Muft na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir leo ameutangazia umma wa Kiislam Tanzania kwamba leo siku ya Jumapili mwezi umeandama na umeonekana maeneo mbalimbali nchini. hivyo kesho siku ya Jumatatu ni sikukuu ya Idd.”