Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Akamatwa kwa madai ya kulawiti, kuua

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro

Muktasari:

  • Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamshikilia mtu mmoja mwenye umri wa miaka 16 (jina limehifadhiwa) kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa miaka minne na kumsababishia kifo.


Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamshikilia mtu mmoja mwenye umri wa miaka 16 (jina limehifadhiwa) kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa miaka minne na kumsababishia kifo.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Novemba 11, 2021 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro imeeleza kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 10, 2021 saa tatu asubuhi huko Chamazi Mbande Wilaya ya Temeke.

Kamanda Muliro amesema uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo unafanyika na hatua za kisheria  zitazingatiwa ili haki, itendeke.