Hatimaye Serikali imesikia kilio cha Watanzania kwa kufuta na kupunguza kiwango cha tozo za miamala ya kieletroniki.

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumanne Septemba 20, 2022 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba bungeni baada ya kipindi cha maswali na majibu.