Kutokana na ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janab ametoa angalizo kuwa licha ya kuharibu bajeti ya afya kila mwaka, maradhi hayo yataathiri uchumi wa familia na nguvukazi ya Taifa.