Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wanahisa wa Benki ya CRDB waridhishwa na uongozi wa Dk Nsekela, wataka aendelee kuingoza benki hiyo

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (katikati) akiongoza Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB. Wengine pichani ni Dk Donald Mmari, Makamu Mwenyekiti ( kulia), Dk Abdulmajid Nsekela, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB (wa pili kushoto), Fredrick Nshekanabo, Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB (wa kwanza kushoto) na Pascal Mihayo, Katibu wa Benki na Mkurugenzi wa Sheria wa Benki ya CRDB.

Wanahisa wa Benki ya CRDB wameele­za matumaini yao ya kuona Mkurugenzi Mtendaji, Dk Abdulmajid Nsekela akien­delea kuiongoza wa Benki hiyo hata baada ya ukomo wa kawaida wa miaka 10 ya uon­gozi, wakiamini kuwa bado ana nguvu, maono, uzoefu na uwezo mkubwa wa kuen­delea kuipeleka benki hiyo katika hatua nyingine ya mafanikio makubwa zaidi.

Wanahisa hao wana­eleza kuwa sababu kub­wa inayowafanya kuwa na imani kubwa na uongozi wa Dk Nsekela ni kiwan­go kikubwa cha thamani ambacho wamekipata kupi­tia uwekezaji wao ndani ya Benki ya CRDB katika kipindi chake cha uongozi.

Wakati Dk Nsekela ana­chukua uongozi wa Benki ya CRDB mwaka 2018, tha­mani ya hisa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam iliku­wa wastani wa Sh 95 kwa hisa, lakini kufikia Aprili mwaka 2026 thamani hiyo ilikuwa imefikia wastani wa Sh 3,000 kwa hisa, hat­ua ambayo wanahisa wen­gi wanaielezea kama moja ya safari kubwa zaidi ya ukuaji wa thamani kuwahi kushuhudiwa katika sekta ya fedha nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk Abdulmajid Nsekela akiwasilisha taarifa ya Menejimenti kwa mwaka 2025 katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa wa Arusha (AICC), Mei 16, 2026.

Kwa upande wa gawio, mwaka 2018 wanahisa walil­ipwa Shilingi 5 kwa hisa, lakini kutokana na matokeo makubwa ya kihistoria yaliy­opatikana mwaka jana 2025, wanahisa walipitisha gaw­io la Sh 90 kwa kila hisa, sawa na ongezeko la zaidi ya asilimia 1000. Benki hiyo pia imeendelea kuwa miongoni mwa kampuni zenye thama­ni kubwa zaidi katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), ikiwa na thamani ya soko inayozidi Dola za Marekani bilioni 2.8, jambo ambalo limeendelea kuongeza imani ya wawekezaji wa ndani na nje ya Tanzania.

Mzee Godfrey Mosha mmoja ya wanahisa waanzil­ishi wa Benki ya CRDB tokea mwaka 1996 amesema tokea awe mwanahisa hajawahi kushuhudia ukuaji mkubwa wa thamani ya wanahisa na biashara ya benki hiyo kama ambavyo imetokea kati­ka kipindi cha uongozi wa Dkt. Nsekela. “Hakika tume­shuhudia ukuaji wa ajabu na wakihistoria katika sekta ya fedha nchini,” alisema.

“Licha ya faida ya benki yetu kuongezeka kwa zaidi ya asilimia 1000 tangu Dk Nsekela alipochukua hata­mu ya uongozi, jumla ya mali za Benki ya CRDB zimefikia Sh 23.9 trilioni mwaka 2026 kutoka takribani Sh 7.6 trili­oni mwaka 2018.

Viongozi wastaafu wa Benki ya CRDB wakifuatilia kwa karibu taarifa ya wakurugenzi na Ripoti ya Fedha kwa mwaka 2025 wakati wa Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB. Kutoka kushoto ni Martin Mmari, Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dk Ally Laay, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, na Dk Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa Benki ya CRDB.

Amana za wateja zime­ongezeka kutoka takribani Shilingi trilioni 4.8 mwaka 2018 hadi kufikia Sh 16.2 tri­lioni, mikopo ikikua kutoka takribani Sh 3.6 trilioni hadi kufikia Sh 14.7 trilioni. Huu ni ukuaji wa ajabu hatupaswi kumuacha kijana huyu aon­doke mapema wakati bado ana nguvu za kutupelekea katika mafankio zaidi,” alisema Mzee Mosha katika Mkutano huo Mkuu wa 31 wa Wanahisa.

Taarifa ya mwaka ya Benki ya CRDB inaonyesha ukua­ji huu umeifanya Benki ya CRDB kuendelea kuongoza soko la fedha nchini ikishika soko la benki kwa asilimia 28 ya amana zote za wateja nchini, asilimia 27 ya mali zote za sekta ya benki, asili­mia 29 ya mikopo iliyotolewa na taasisi za fedha pamoja na asilimia 30 ya faida baa­da ya kodi miongoni mwa zaidi ya benki 40 zilizopo nchini. Kwa wanahisa wen­gi, takwimu hizi si tu alama ya mafanikio ya biashara, bali ni ushahidi wa uongozi wenye maono makubwa na uwezo wa kutekeleza mika­kati kwa ufanisi.

Katika Mkutano huo Mkuu, sauti ya wanahisa ilikuwa moja; pongezi kwa matokeo yaliyopatikana na matu­maini makubwa kuhusu mustakabali wa benki hiyo. Wengi wao walieleza kuwa mafanikio yaliyopatikana ndani ya kipindi cha miaka minane iliyopita yanaonye­sha wazi namna ambavyo uongozi imara, wenye mao­no na uthubutu unavyoweza kubadilisha taasisi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori akiwasilisha taarifa yake kwa mwaka 2025 katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa wa Arusha (AICC), Mei 16, 2026 ambapo Bodi ya Wakurugenzi iliwasilisha pendekezo la gawio la Sh. 90 kwa hisa ambalo lilipitishwa kwa pamoja na wanahisa.

Akizungumza katika mkutano huo Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye alisema “Katika ulimwen­gu wa fedha duniani kote, Afisa Mtendaji Mkuu kama hana matatizo na anafanya vizuri kwa viwango hivi vya Dk Nsekela huwa hawam­badilishi kirahisi kwa saba­bu ukimbadilisha hisa zin­ashuka, lakini pia utendaji wa taasisi unaweza kushuka kwa sababu imani ya wateja na wawekezaji wengi mara nyingi ipo kwenye maono na uongozi imara unaonyeshwa na Afisa Mtendaji Mkuu.”

Wanahisa wengi wame­kuwa wakitaja mkakati wa biashara wa “Evolve” kama moja ya hatua muhimu zaidi zilizobadilisha sura ya Benki ya CRDB. Kupitia mkakati huo wa miaka mitano (2023/27), Benki hiyo imefanikiwa kuimarisha mifu­mo ya kidijitali, kuongeza ujumui­shi wa kifedha, kupanua huduma zake nje ya mipaka ya Tanzania, kuboresha uzoefu wa wateja na kuongeza thamani kwa wanahisa kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa hapo awali.

Hivi sasa, zaidi ya asilimia 98 ya miamala yote ya benki hiyo inafanyika nje ya matawi, hatua inayoonyesha mafanikio makub­wa ya uwekezaji katika teknolojia. Aidha, asilimia 50 ya akaunti mpya sasa zinafunguliwa kupitia majuk­waa ya kidijitali huku asilimia 40 ya miamala yote ikifanyika nje ya muda rasmi wa kazi wa matawi. Mabadiliko haya yameifanya Benki ya CRDB kuwa moja ya taasisi za fedha zilizoongoza katika mageuzi ya kidijitali Afrika Mashariki.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Fredrick Sumaye akichangia mada katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa wa Arusha (AICC), Mei 16, 2026.

Benki ya CRDB pia imeendelea kupanua ushawishi wake nje ya Tanzania. Kupitia uwekezaji kati­ka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Burundi pamoja na uwepo wake Dubai, benki hiyo imeendelea kuwa daraja muhimu la biashara linalounganisha Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, Ghuba ya Uarabuni pamoja na masoko ya Asia. Hatua hiyo imeongeza fursa kwa wafanyabiashara, wawekeza­ji na wajasiriamali wa Tanzania kupata masoko mapya ya kikanda na kimataifa.

Katika umri wa miaka 54 pekee, wengi wanaamini kuwa Dk Nseke­la bado ana nguvu, uzoefu, maono na uwezo wa kuendelea kuiongoza benki hiyo kuelekea hatua nyingine kubwa zaidi ya ukuaji. Wanaami­ni kuwa baada ya mafanikio ya mkakati wa “Evolve” unaotaraji­wa kukamilika mwaka 2027, ben­ki hiyo ina nafasi kubwa zaidi ya kufanya mageuzi makubwa katika ukanda wa Afrika ikiwa itaendelea kujengwa juu ya msingi imara wa uongozi, ubunifu na nidhamu ya kiutendaji.

“Tunaimbo Serikali yetu sikivu, itusikilize sisi wanahisa wa Benki ya CRDB kwani bado tunaimani na Dk Nsekela anauwezo wa kutu­fikisha katika mafanikio makubwa zaidi tunapoelekea kuanza na kute­keleza mkakati mpya wa biasha­ra utakaoanza mwaka 2028/32,” amesema Mzee Chedego moja ya wanahisa waanzilishi huku akise­ma kwa utendaji alioonyesha Dk Nsekela ni ngumu kwa wanahisa kumuacha aondoke.

Mwanahisa mwanzilishi wa Benki ya CRDB, Godfrey Mosha akitoa mchango wake katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimatifa wa Arusha (AICC), Mei 16, 2026. Mzee Mosha ni kati ya wanahisa wengi ambao wamependekeza Dk Nsekela kuendelea kuongoza Benki hiyo kutokana na mafanikio makubwa ambayo benki hiyo imeyapata tokea aliposhika hatamu.

Hata hivyo, wanahisa hao wana­heshimu sheria zilizowekwa na serikali pamoja na mamlaka za udhibiti, na kusema kuwa maom­bi yao ni kwa maslahi mapana ya Benki yao ya CRDB na mus­takabali mpana wa sekta ya fedha na Taifa kwa ujumla. Maombi ya wanahisa yameungwa zimeungwa mkono pia na baadhi ya viongo­zi wastaafu wa sekta ya fedha na wanahisa wakubwa akiwamo Dkt. Charles Kimei pamoja na Dk Ally Laay, ambao wamekuwa wakieleza kuvutiwa kwao na kasi ya ukuaji, uthabiti wa utendaji wa Benki yao.

Katika robo ya kwanza ya mwa­ka 2026, Benki ya CRDB imeand­ika historia mpya kwa kuongoza katika viashiria vyote vikuu vya kiutendaji nchini. Benki hiyo ili­rekodi faida baada ya kodi ya Sh 206 bilioni, kiwango kikubwa zaidi kuwahi kufikiwa na benki nchini ndani ya robo ya kwanza.

Kampuni zake tanzu nazo zimeendelea kufanya vizuri amba­po CRDB Bank Burundi ilipata faida ya Sh 12.9 bilioni, CRDB Bank DR Congo faida ya Sh 828 milioni huku CRDB Insurance ikirekodi faida ya Sh 1.8 bilioni. Kwa upande wa CRDB Bank Foundation, imeen­delea kuwa chombo muhimu cha uwezeshaji wa wananchi nchi­ni kupitia programu ya IMBEJU, huku zaidi ya wanufaika milioni 1 wakiwezeshwa.

Katika mazingira hayo ya utendaji, wanahisa wameadhimia kuunda jopo la ushauri linaloon­gozwa na Mzee Gachuma kwa len­go la kuwasilisha maoni yao kwa heshima na kwa kufuata taratibu zote stahiki kwa serikali kuhusu matarajio yao ya kuona uzoefu na maono ya Dk Nsekela yakiendelea kuisaidia benki hiyo katika hatua inayofuata ya ukuaji.

Kwa wanahisa wengi, mjadala huu hauhusu mtu mmoja pekee, bali unahusu uthabiti wa taasi­si, mwendelezo wa mafanikio na kulinda kasi ya ukuaji ambayo imeifanya Benki ya CRDB kuwa taasisi ya mfano katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.