Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Siku ya Hedhi Salama 2025: Safari ya ujenzi wa mazingira salama kwa hedhi kwa kila mwanamke na msichana

Mkurugenzi Mkazi wa WaterAid Tanzania, Anna Mzinga.

Katika kuadhimisha Siku ya Hedhi Salama Duni­ani mwaka 2025 chini ya kaulimbiu “Kwa Pamoja kwa Hedhi Salama," Water­Aid Tanzania imeweka wazi malengo yake ya kuhakiki­sha kila mwanamke na msi­chana nchini anaishi katika mazingira yanayomuweze­sha kujistiri kwa staha na usalama wakati wa hedhi.

Mazingira salama kwa ajili ya hedhi sio tu wazo lililopo hewani, bali ni len­go linalotekelezeka ambalo msingi wake unaanzia kwe­nye upatikanaji wa uhakika wa maji safi, vyoo vyenye staha, sehemu za kujistiri na taarifa sahihi.

Kuanzia mashuleni, vituo vya afya hadi maeneo ya masoko, WaterAid Tanzania inapambana kupaza sauti, kuboresha upatikanaji wa huduma za maji safi na usafi wa mazingira, na kuhakiki­sha kuwa hedhi haiwi kik­wazo katika elimu, mahala pa kazi au ushiriki wa wan­awake na wasichana katika jamii zao.

Mkurugenzi Mkazi wa WaterAid Tanzania, Anna Mzinga amefanya mazun­gumzo na mwandishi wa gazeti hili kuhusiana na siku hiyo na alikuwa na majibu yafuatayo:-


Kaulimbiu ya Siku ya Hedhi Salama ya mwaka huu ni "Kwa Pamoja kwa Hedhi Salama." Mazingira salama kwa hedhi yanabeba tafsiri gani kwa WaterAid Tanza­nia?

Anna: Mazingira salama kwa hedhi ni ile hali ambayo kila mwanamke na msichana anaweza kujistiri kwa usal­ama, staha na usafi – hali inayoongeza kujiamini kwao bila kulazimika kukatisha masomo, kusimama kufanya kazi au kuishi kwa uhuru katika jamii. Kwa WaterAid Tanzania, hii inamaanisha wanawake na wasichana wanaweza kupata huduma muhimu kama maji safi, vyoo rafiki kwa makundi ya jinsi zote, na taarifa sahihi kuhusu afya ya hedhi.

Wanawake na wasichana wanaposhindwa kuhud­huria masomo au kuingia kazini kwa sababu ya hedhi, hupoteza fursa ya kujifunza, kujipatia kipato, na kuleta mabadiliko. WaterAid Tan­zania tunahakikisha shule, vituo vya afya na maeneo ya umma yanapata huduma muhimu kama maji safi, vyoo bora, vifaa vya kunawa mikono, maeneo ya faragha kwa ajili ya kujistiri wakati wa hedhi, na taarifa sahihi zenye msaada vyote hivi kwa njia endelevu.

Miundombinu ya umma inaposaidia afya ya hedhi, wasichana wataweza kuhud­huria shule mara kwa mara na wanawake wataweza kwenda kazini na kuishi kwa staha katika jamii. Tunaami­ni hili ni jambo muhimu kwa kufanikisha usawa wa kijin­sia na maendeleo jumuishi nchini mwetu.


Kwa nini rasilimali maji ni muhimu katika kufikia hedhi salama?

Anna: Maji ni msingi wa hedhi salama. Kupitia maji, wanawake na wasichana wanaweza kunawa mikono, kusafisha miili yao, na kuji­hisi safi na huru wakati wa hedhi. Bila maji safi, kujistiri wakati wa hedhi huwa ni jambo hatarishi, linaloko­sesha amani na linaloweka rehani utu wa mtu. Mashu­leni, sehemu za kazi, maso­ko, na vituo vya afya, upati­kanaji wa maji ya uhakika ni msingi wa mazingira salama ya hedhi.

Linapokuja suala la hedhi salama, kwa nini unadhani vyoo bora vinamuwezesha mwanamke au msichana kushiriki na kujitokeza mahala popote mbele ya jamii?

Anna: Vyoo bora ambavyo ni sala­ma, safi, vyenye faragha na vina­vyopatikana kwa urahisi vinamwezesha msichana au mwanamke kujistiri wakati wa hedhi bila uwoga wala aibu. Tunapokuwa na vyoo vyenye maji na sehemu za kutupa taulo za kike, tuna­onyesha utu na ulinzi.

Wasichana wana uweze­kano mkubwa wa kuhudhu­ria masomo na kubaki shu­leni, na wanawake kuende­lea kufanya kazi na kushiriki katika masuala ya kijamii kwa uhuru. Ni hatua rahisi lakini yenye nguvu katika kuelekea usawa wa kijinsia na ushirikishwaji.


Swali: Tuambie zaidi kuhusu jitihada za WaterAid Tanza­nia, hususan zinazohusiana na afya ya hedhi mashuleni na katika vituo vya afya

Anna: WaterAid Tanzania tunahakikisha shule na vituo vya afya vina maji safi, vyoo bora na usafi binafsi. Mashu­leni, tumejenga vyoo rafiki kwa makundi ya jinsi zote vyenye vituo vya kunawa mikono na maeneo ya far­agha kwa ajili ya hedhi sal­ama. Katika vituo vya afya, kazi yetu ni kuhakikisha wafanyakazi wa kike, wag­onjwa na walezi wanakuwa kwenye mazingira salama wanapojistiri wakati wa hedhi. Jitihada hizi zime­ongeza mahudhurio, faraja, na utu hususan kwa wasi­chana balehe na wanawake.


Tuambie zaidi kuhusu MHM kwa wasichana shu­leni na namna klabu za SWASH zinavyosaidia kubadilisha hali ili­yopo

Anna: Usimamizi wa Hedhi Mashu­leni (MHM) una nafasi muhimu katika kuwafanya wasichana wabaki darasani, kuongeza ufaulu na kujiamini. Klabu za SWASH (Vikundi vya Huduma za Maji Safi, Vyoo Bora na Usafi Binafsi Mashuleni) huhamasi­sha usafi, huon­geza uele­wa kuhusu hedhi, na kutoa msaada wa rika.

Klabu hizi husaidia kuvunja ukimya, kurahisisha mazungumzo kuhusu afya ya hedhi, na kuhakikisha mazingira ya shule yanaki­dhi mahitaji ya wasichana – na wavulana pia. Katika maeneo yenye klabu za SWASH, tumeona ongezeko la kujiamini miongoni mwa wasichana na mahudhurio ya mara kwa mara shuleni hata wakati wa hedhi, pamo­ja na kuboresha utamaduni wa kuzingatia usafi mion­goni mwa wanafunzi.


Changamoto zipi jamii ina­kutana nazo kuhusu hedhi salama, hususan wanawake walioko kwenye jamii hizo? Na WaterAid Tanzania inak­abiliana nazo vipi?

Anna: Maeneo mengi ya umma kama masoko, vituo vya mabasi na vituo vya kijamii hayana maji safi wala vyoo vinavyofanya kazi. Hii inawafanya wanawake washindwe kujistiri wakati wa hedhi wakiwa kazini au katika shughuli zao za kila siku, hivyo wanalazimika kubaki nyumbani au kutu­mia njia mbadala ambazo ni hatari­shi.

WaterAid hivi karibuni tumekabidhi vyoo rafiki kwa makundi ya jinsi zote katika masoko mawili ya Ngaram­toni, jijini Arusha. Hatua hii imeongeza kujiamini, usala­ma na ushiriki wao wafanya­biashara wanawake katika uchumi.


Ungependa watu waelewe nini kuhusu afya ya wan­awake hususan katika Siku ya Hedhi Salama Duniani kwa mwaka 2025? (Wito kwa jamii)

Anna: Wanawake wanahi­taji huduma bora: Kampeni ya What Women Want ili­pohoji wanawake milioni 1.2 duniani kote, ikiwemo Tanzania, kuhusu kile wanachotaka kutoka kwe­nye huduma za afya ya uzazi na mama, walitaja huduma zenye staha, maji safi, vyoo bora na usafi wa mazingira kama vipaumbele vyao vya msingi.

Kwa kuwa wanawake wako hatarini kupata maam­bukizi, hivyo kuhimiza hedhi salama kunachangia kui­marisha afya yao kwa ujum­la, ikiwa ni pamoja na afya ya uzazi na afya ya vijana balehe.


Kama ungepata nafasi moja ya kutoa rai kwa Mamlaka zenye nafasi ya kushughu­likia jambo hili, ingekuwa ni ipi?

Anna: Serikali zina uwezo wa kuleta mabadi­liko ya kweli. Na vyombo vya habari vina uwezo wa kuzifanya zisikilize kero. Ninatoa wito kwa wadau wa maendeleo katika sekta za afya, elimu, jinsia na WASH pamoja na Serikali ya Tan­zania kuwekeza fedha katika maji safi, vyoo bora, huduma za usafi kati­ka shule, maeneo ya umma na vituo vya afya — ili kila mwa­namke na msichana aweze kujitokeza na kush­iriki kwe­nye shu­ghuli za kiuchumi kwa mafani­kio mahala popote, muda wowote ule.


Hadithi za mafanikio

Safari ya binti mmoja: Kutoka kuwa na aibu hadi kuwa na ndoto

Katika shule ya msingi iliyopo katika kijiji cha Laghanga, ipo habari ya binti mmoja ambaye alikuwa ana­kosa amani pindi tu mzun­guko wake wa hedhi unapo­fika. Shuleni kwao hakukuwa na maji safi, vyoo vilikuwa vichafu mno na hakukuwa na vyumba maalumu vya wasi­chana kujistiri.

Leo hii, kila kitu kimebadi­lika. Nyuma ya haya mab­adiliko yote yupo Shirika la WaterAid Tanzania, kupi­tia mradi wao usambazaji huduma za maji safi, vyoo bora na usafi wa mazingira (WASH) ambapo shule yao imebahatika kupata vyoo rafiki kwa makundi ya jinsi zote, vyumba vya kubadil­ishia taulo za kike, vituo vya kunawia mikono na huduma za uhakika za maji safi.


Sauti ya mwalimu aliyevunja ukimya

Katika Wilaya ya Kisarawe, yupo mwalimu aliyeamua kupaza sauti katika jamii ambayo kuzungumzia masu­ala ya hedhi ni mwiko mpaka pale sherehe za kimila zita­kapofanyika (ngoma).

Kupitia klabu za shule za mradi wa WASH, hivi sasa anaelimisha vijana (wasi­chana na wavulana) kuhusu masuala ya hedhi salama. Uthubutu wake umekuwa na mchango mkubwa katika kujenga uelewa wa vijana kuhusu afya ya hedhi.

“Licha ya uwepo wa mila ya ‘ngoma’ inayozuia mazungumzo kuhusu hedhi, mimi hukaa na wasichana na kuzungumza nao. Kupitia klabu ya WASH, navunja uki­mya. Wasichana wanapata taarifa sahihi kunakowa­jengea kujiamini na kuuliza maswali,” anasema Grace.


Uwezeshaji wanawake mae­neo ya masoko

Jitihada za WaterAid Tanzania haziishii mashu­leni, bali zinakwenda hadi kwa wanawake na wasi­chana waliopo maeneo ya masoko. Wilayani Arusha, kwenye maeneo ya Oltrumet na Olmotony, vyoo viwili vya kisasa (vyoo rafiki kwa makundi ya jinsi zote) vili­jengwa vikihudumia watu­miaji wa masoko zaidi ya 1000 kila siku.

Vyoo vina nafasi kwa wan­awake na wasichana katika masoko kutumika wakati wa mizunguko yao ya hedhi vikiwa na maeneo ya kuhi­fadhia taka, kuvifanya kuwa si tu vyoo bali ni ishara ya utu, afya na fursa.