Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumapili, Machi 9, 2025 amezindua mradi wa maji wa Same -Mwanga – Korogwe katika mikoa ya Kilimanjaro na Tanga. Uzinduzi huo uliofanyika Mwanga mkoani Kilimanjaro, pia umeshuhudiwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso na Waziri Mkuu mstaafu, Cleopa Msuya.