Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga yatawala tuzo Ligi Kuu

Muktasari:

  • Dube ameibuka mchezaji bora wa mwezi akiwashinda kiungo wa timu yake, Stephanie Aziz KI na mshambuliaji wa KenGold, Selemani Bwenzi.

Mshambuliaji wa Yanga, Prince Dube na kocha wake, Miloud Hamdi wamebeba tuzo za ubora za Ligi Kuu Bara mwezi Februari.

Dube ameibuka mchezaji bora wa mwezi akiwashinda kiungo wa timu yake, Stephanie Aziz KI na mshambuliaji wa KenGold, Selemani Bwenzi.

Ndani ya Februari, Dube, raia wa Zimbabwe alikuwa wa moto ambapo kwenye mechi saba alizotumia dakika 562 alifunga mabao matano na kutoa asisti tano akihusika kwenye jumla ya mabao 10.

Wakati Dube akitamba hivyo, Hamdi amebeba tuzo yake ya kwanza ya kocha bora akiwashinda Fadlu Davids wa Simba na Fred Minziro wa Pamba Jiji aliochuana nao.

Hamdi aliiongoza Yanga kushinda mechi nne za ligi akiifanya Yanga kukusanya pointi 12.

Ndani ya mechi hizo walizifunga  KMC, Singida Black Stars, Mashujaa na Pamba Jiji - Yanga ikifunga jmabao 16 huku ikiruhusu mawili.