Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Chelsea inavyofaidi upana wa Kikosi

Muktasari:

  • Chelsea ilipata ushindi huku wachezaji kama Noni Madueke, Enzo Fernandez, Jadon Sancho na Nicolas Jackson wote wakibaki England, wakati Cole Palmer mfungaji wao bora katika Ligi Kuu ya England, akiwa hayumo katika kikosi cha Europa Conference.

Chelsea imeendelea kuonyesha ubora wake baada ya kupata ushindi wa tano mfululizo ikiifunga Astana mabao 3-1 ikiwa ugenini kwenye uwanja wa Ortalyq katika michuano ya Europa Conference.

Licha ya kupumzisha wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza kocha wa Chelsea Enzo Maresca alifanikiwa kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mabingwa hao wa Kazakhstani ambao wamekuwa na wakati mgumu katika mashindano haya ambapo wanashika nafasi ya 28 wakiwa wameshinda mechi moja, sare moja, huku wakipoteza mechi tatu kati ya tano walizocheza.

Mabao ya Chelsea yalifungwa na Marc Guiu dakika ya 14 akifunga bao la kwanza kabla ya kufunga bao lingine dakika ya 19 huku Renato Veiga akifunga bao la tatu dakika ya 40 ambapo bao la kufuta machozi la Astana lilifungwa dakika ya 45 kabla ya mapumziko kwa shuti kali lililopigwa na nahodha Marin Tomasov.

Wachezaji wa kikosi cha pili pamoja na wale waliyopangwa kutoka kituo cha kukuzia vipaji cha Cobham ambao walicheza mechi yao ya kwanza kwenye mashindano ya Ulaya walipambana na kuonyesha mchezo mzuri ambapo mpaka dakika 90 zinamalizika Chelsea iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Wachezaji kama Noni Madueke, Enzo Fernandez, Jadon Sancho na Nicolas Jackson wote walibaki England, huku Cole Palmer mfungaji wao bora katika Ligi Kuu ya England, akiwa hayumo katika kikosi cha Europa Conference.

Hali hiyo ilimfanya Marc Guiu, mwenye umri wa miaka 18, kuongoza safu ya ushambuliaji, huku Sam Rak-Sakyi (19), Josh Acheampong (18) na Tyrique George (18)   wakianza kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha kwanza katika historia ya Chelsea kuanza na wachezaji wanne wa umri mdogo katika mashindano ya Ulaya.

Kuanzishwa kwa Shim Mheuka kulimfanya kuwa mchezaji wa pili mwenye umri mdogo zaidi kucheza kwenye mashindano ya Ulaya akiwa na miaka 17 na siku 54 baada ya Dominic Solanke kuwahi kufanya hivyo alipokuwa Chelsea.

Rak-Sakyi alionyesha utulivu na umahiri akiwa na mpira, bila shaka alionyesha kiwango bora kwenye eneo la kati ambapo wamekuwa wakicheza Moises Caicedo na Romeo Lavia.


Kikosi cha Chelsea dhidi ya Astana

Golipa: Filip Jorgensen

Mabeki: Joshua Acheampong, Tosin Adarabioyo, Axel Disasi, Renato Veiga

Viungo: Rak-Sakyi, Dewsbury-Hall, Carney Chukwuemeka

Washambuliaji: Pedro Neto, Marc Guiu, Tyrique George


Matokeo ya mechi nyingine

Astana 1-3 Chelsea

Fiorentina 7-0 LASK

Copenhagen 2-0 Hearts

Dinamo-Minsk 2-0 Larne

Noah 1-3 APOEL

Petrocub 0-1 Real Betis

HJK Helsinki 2-2 Molde

İstanbul Başakşehir 3-1 Heidenheim

Legia Warszawa 1-2 Lugano

Olimpija Ljubljana 1-4 Cercle Brugge

St. Gallen 1-4 Vitória SC

Mladá Boleslav 1-0 Jagiellonia Białystok

Gent 3-0 TSC

Omonoia 3-1 Rapid Wien

Pafos 2-0 Celje

Shamrock Rovers 3-0 Borac

The New Saints 0-2 Panathinaikos

Víkingur Reykjavík 1-2 Djurgården