Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Amorim kufukuzia rekodi leo

Muktasari:

  • Mara ya mwisho United ilicheza dhidi ya Sparta Prague mwaka 2004 ambapo mchezo ulimalizika kwa sare ya 0-0 huku ikisubiriwa leo kama wataweza kupata ushindi wa kwanza wakiwa nchini humo.

Meneja wa Man United Ruben Amorim huwenda akaweka rekodi ya kuiongoza United kupata ushindi kwenye aridhi ya Jamuhuri ya watu wa Czech dhidi ya Viktoria Plzen katika mchezo wa Ligi ya Europa.

Mara ya mwisho United ilicheza dhidi ya Sparta Prague mwaka 2004 ambapo mchezo ulimalizika kwa sare ya 0-0 huku ikisubiriwa leo kama wataweza kupata ushindi wa kwanza wakiwa nchini humo.

United inaingia kwenye mchezo wa leo ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kutoka kupoteza mechi mbili za Ligi Kuu England ambapo ilipoteza mabao 2-0 dhidi ya Arsenal huku ikipoteza mabao 3-2 ikiwa nyumbani dhidi ya Nottingham Forest, Desemba 8, 2024.

Manchester inashika nafasi ya 12, ikiwa na pointi tisa kwenye michezo mitano iliyocheza sawa na Viktoria Plzen ambayo inashika nafasi ya 13 ikiwa na pointi tisa huku United ikiizidi tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa ikiwa imefunga mabao 10 ikiruhusu mabao saba wakati Viktoria Plzen imefunga mabao tisa ikiruhusu mabao saba.

Iwapo leo, United itapata matokeo mazuri itafikisha michezo sita bila kupoteza kwenye mashindano haya ambapo Ruben Amorim atakuwa kocha wa kwanza kuongoza mechi sita za mashindano ya Ulaya bila kupoteza tangu alipofanya hivyo David Moyes akiwa na Manchester United msimu wa 2013-2014.


Mechi nyingine za Leo

AS Roma vs Braga

Viktoria Plzen vs Manchester United

Malmö FF vs Galatasaray

Olympiacos vs FC Twente

PAOK vs Ferencvaros

Ludogorets Razgrad vs AZ Alkmaa

Union Saint-Gilloise vs Nice

TSG Hoffenheim vs FCSB

Ajax vs Lazio

FC Porto vs FC Midtjylland

FCSB vs Olympiacos

Bodo/Glimt vs Besiktas

IF Elfsborg vs FK Qarabag

Maccabi Tel-Aviv vs Rigas Futbola Skola

Lyon vs Eintracht Frankfurt

Rangers FC vs Tottenham Hotspur

Real Sociedad vs Dynamo Kyiv

Slavia Prague vs Anderlech