Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Chelsea kuendeleza ubabe Conference Ligi

Muktasari:

  • Chelsea imeondoka na wachezaji wengi chipukizi huku ikiwaacha wachezaji wazoefu kama Christopher Nkunku, João Félix, Benoît Badiashile, na Mykhaylo Mudryk huku Maresca akitaja kuwapa nafasi wachezaji chipukizi kwenye mchezo wa leo.

Chelsea itashuka dimbani kwenye uwanja wa ugenini leo dhidi ya Astana kwenye mchezo wa Europa Conference Ligi ambapo imekuwa na mwendelezo mzuri wa matokeo kwenye michuano hii.

Kocha Enzo Maresca ameiongoza Chelsea kupata ushindi kwenye michezo minne iliyocheza ambapo inaongoza kwenye msimamo wa Conference Ligi ikiwa na pointi 12 sawa na Legia Warszawa ambayo nayo haijapoteza mchezo kwenye mashindano hayo.

Kikosi cha Enzo Maresca kilifanikiwa kushinda dhidi ya Gent mabao 4-2, Panathinaikos 4-1, na FC Noah 8-0 kabla ya kuwashinda Heidenheim kutoka Ujerumani kwa mabao 2-0 ambayo yalifungwa na Christopher Nkunku dakika ya 51 na bao la dakika za mwisho lililofungwa na Mykhaylo Mudryk.

Chelsea imeondoka na wachezaji wengi chipukizi huku ikiwaacha wachezaji wazoefu kama Christopher Nkunku, João Félix, Benoît Badiashile, na Mykhaylo Mudryk huku Maresca akitaja kuwapa nafasi wachezaji chipukizi kwenye mchezo wa leo.

Tofauti na Ligi ya Mabingwa Ulaya na ile ya Europa ambapo timu zinacheza mechi nane kwa mfumo wa nyumbani na ugenini, timu za Conference League zina mechi sita pekee kwenye ratiba zao ambapo Chelsea ipo kileleni mwa Conference Ligi yenye timu 36.

Chelsea itaingia kwenye mchezo wa leo ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kucheza mechi nane bila kupoteza kwenye mashindano yote tangu ilipofungwa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle United kwenye EFL Cup Oktoba 30, 2024.

Chelsea pia wameshinda mechi zao nne za ugenini mfululizo, ikiwemo ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Tottenham Hotspur kwenye Ligi Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita. Ushindi huo umewapandisha hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi kuu England wakiwa pointi nne nyuma ya vinara Liverpool wenye pointi 35 ambao wana mechi moja mkononi.

Astana imeonekana kuwa na hali mbaya kwenye mashindano haya baada ya kupata ushindi mara moja wa bao 1-0 dhidi ya Backa Topola huku ikitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Vitoria Guimaraes ikiwa imepoteza mechi mbili ambapo ilifungwa mabao 2-0 dhidi ya The New Saints kabla ya kufungwa tena bao 1-0 dhidi ya Pafos.


Mechi nyingine za leo

Astana vs Chelsea

Fiorentina vs LASK

Copenhagen vs Hearts

Dinamo-Minsk vs Larne

Noah vs APOEL

Petrocub vs Real Betis

HJK Helsinki vs Molde

İstanbul Başakşehir vs Heidenheim

Legia Warszawa vs Lugano

Olimpija Ljubljana vs Cercle Brugge

St. Gallen vs Vitória SC

Mladá Boleslav vs Jagiellonia Białystok

Gent vs TSC

Omonoia vs Rapid Wien

Pafos vs Celje

Shamrock Rovers vs Borac

The New Saints vs Panathinaikos

Víkingur Reykjavík vs Djurgården