Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Watatu wajeruhiwa ajalini katika msafara wa Makamu wa Rais

Picha na Haiko Kimaro

Muktasari:

Ajali asubuhi leo mbele kidogo ya Nijiji cha Nanguruwe na majeruhi ambao ni dereva na wasaidizi wa makamu rais, wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa Ligula.

Mtwara. Watu watatu wamejeruhiwa baada ya gari moja katika msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani uliokuwa unaelekea wilayani Tandahimba mkoani Mtwara kupinduka.

Ajali hiyo imetokea asubuhi leo mbele kidogo ya kijiji cha Nanguruwe na majeruhi ambao ni dereva na wasaidizi wa makamu rais, wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa Ligula.

Kabla  ya ajali hiyo, gari jingine lililokuwa limebeba baadhi ya waandishi wa habari, Channel ten, Clouds tv na Star TV iliacha njia na kugonga kwenye kingo za barabara lakini hakuna aliyepata madhara.