Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ulikuwa uamuzi mgumu ujenzi daraja la Ubungo

#LIVE​: RAIS MAGUFULI AKIZINDUA FLYOVER YA UBUNGO || KITUO CHA MABASI MBEZI LUIS

Muktasari:

  • Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) ambaye pia ni mbunge wa  Ubungo, Profesa Kitila Mkumbo amesimulia namna uamuzi mgumu wa  Rais wa Tanzania,  John Magufuli yalivyokamilisha ujenzi wa daraja la juu la Ubungo ‘Kijazi Interchange’.

Dar es Salaam. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uwekezaji) ambaye pia ni mbunge wa  Ubungo, Profesa Kitila Mkumbo amesimulia namna uamuzi mgumu wa  Rais wa Tanzania,  John Magufuli yalivyokamilisha ujenzi wa daraja la juu la Ubungo ‘Kijazi Interchange’.

Profesa Mkumbo ameyasema hayo leo Jumatano Februari 24, 2020 mbele ya Rais Magufuli aliyezindua daraja hilo  katika ziara yake ya siku tatu jijini Dar es Salaam.

“Mradi huu unanigusa sana kwa sababu mwaka 2018 nikiwa Kahama saa 4 usiku nilipokea wito kwamba Rais Magufuli anatuita kesho yake Ikulu saa 4 asubuhi, nikiwa na wasaidizi wangu nilitafuta gari mpaka Mwanza asubuhi tulipanda ndege Mwanza mpaka jijini Dar es Salaam na saa 4 asubuhi  tukawasili.”

“Ulituambia jambo moja tu kwamba naona nyie kubomoa jengo la wizara ya maji na jengo la Tanesco imewashinda sasa nimewaita kuwaambieni kwamba katika masaa sita yajayo, kama hamjabomoa basi nitakuja kubomoa kwa mikono yangu,” amesema Profesa Mkumbo ambaye wakati wa kuanza ujenzi wa daraja hilo alikuwa katibu mkuu Wizara ya Maji ambayo majengo yake yalikuwa jirani na lilipo daraja hilo.

Huku akizungumza kwa umakini  Profesa Mkumbo amesema, “ nakumbuka tulikuwa na Mfugale (Patrick- mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania Tanroads). Tukaangaliana tukaondoka pale  tukaitana pembeni tunaulizana tufanyeje? Mfugale akasema tukabomoe basi tukaitana na mzee Kamwelwe (Isack) siku mbili tukayabomoa.”

Profesa Mkumbo amesema Rais Magufuli alisema haiwezekani Serikali imechukua uamuzi mgumu kubomoa nyumba za wananchi halafu majengo ya Serikali hayabomolewi.

 “Sifa yako kubwa mheshimiwa Rais ni kusimamia maamuzi yako na ndiyo maana leo tunaona majengo haya yamesimama,” amesema.