TMA yatoa angalizo jipya la mvua kubwa

Wakazi wa Dar es Salaam wakisaidiwa kuvushwa katika eneo lililojaa maji. Jangwani. Picha na Maktaba 

Muktasari:

  • Yasema athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa taarifa ya matarajio ya hali mbaya ya hewa kwa siku tano kuanzia leo Jumatano Aprili 24, 2024 saa 9.30 mchana.

TMA imetoa angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Pia imetoa angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Alhamisi Aprili 25, 2024

TMA imetoa angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

TMA pia imetoa angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Ijumaa Aprili 26, 2024

Mamlaka imetoa angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Arusha, Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga, Simiyu, Kigoma, Tabora na Katavi, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

TMA pia imetoa angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili, kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Jumamosi Aprili 27, 2024

Limetolewa angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya Mkoa wa Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba.

Pia angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Jumapili Aprili 28, 2024

TMA imetoa angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili, kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mamlaka imesema uwezekano wa hali hiyo kutokea ni wastani, sawa na kiwango cha athari zinazoweza kutokea.

TMA imesema athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini.