Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Samia atua Mwanza kushiriki tamasha la utamaduni wa Mtanzania

Samia atua Mwanza kushiriki tamasha la utamaduni wa Mtanzania

Muktasari:

  • Rais Samia Suluhu Hassan amewasili jijini Mwanza kwa helkopta maalum kwa ajili ya  kufunga tamasha la utamaduni wa Mtanzania linalofanyika katika viwanja vya Msalaba Mwekundu vilivyopo karibu na makumbusho ya Bujora wilayani Magu mkoani humo.

Mwanza. Rais Samia Suluhu Hassan amewasili jijini Mwanza kwa helkopta maalum kwa ajili ya  kufunga tamasha la utamaduni wa Mtanzania linalofanyika katika viwanja vya Msalaba Mwekundu vilivyopo karibu na makumbusho ya Bujora wilayani Magu mkoani humo.

Rais Samia amepokewa na  viongozi mbalimbali wa kitaifa na wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakiongozwa na mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Robert Gabriel.

Tamasha hilo lilianza jana Jumanne  Septemba 7, 2021 na linatarajiwa kuhitimishwa leo huku lengo lake likiwa kudumisha, kurithisha na kuutangaza utamaduni wa makabila ya Tanzania.

Mwananchi Digital imepita katika maeneo ya Buzuruga, Igoma na National na kushuhudia wananchi wakiwa wamesimama pembeni mwa barabara tayari kumpokea kiongozi mkuu huyo wa nchi.

Katika tamasha hilo zaidi ya viongozi wa kimila kutoka makabila zaidi ya 120 wamehudhuria huku likisindikizwa michezo ya jadi, ngoma na vyakula vya asili.