Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Samia atuma salamu za pole kifo cha Dk Ndugulile

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kutokana na kifo cha Dk Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika.

Dk Ndugulile amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatano, Novemba 27, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Dk Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, kilichotokea usiku wa kuamkia leo Novemba 27, 2024.”

“Ninatoa salamu za pole kwa familia, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk Tulia Ackson, wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wananchi wa Kigamboni, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote.” Ameandika Rais Samia

Dk Ndugulile alikuwa Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Dunia Kanda ya Afrika (WHO) ambaye alipaswa kuanza majukumu hayo mapya Februari 2025.


Endelea kufuatilia Mwananchi.