Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mikononi mwa polisi akituhumiwa kumuua mama yake mzazi

Mikononi mwa polisi akituhumiwa kumuua mama yake mzazi

Arusha. Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia Patrick Mmasi (24) mkazi wa Njiro Kontena kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi, Ruth Mmasi (40) ambaye ni mfanyabiashara maarufu wa madini.

Limeeleza kuwa baada  ya kufanya mauaji aliutumbukiza mwili katika shimo la choo.

Tukio hilo limebainika juzi baada ya raia wema kutoa taarifa za siri polisi ambao walikwenda na kubaini mwili huo.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa  Arusha, Justine Masejo amesema taarifa rasmi zitatolewa lakini polisi wanamshikilia Patrick kwa tuhuma za mauaji.

"Tunamshikilia kijana huyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani," amesema.

Taarifa kutoka kwa ndugu wa marehemu ambaye hakutaka jina lake kutajwa,  amesema tukio limetokea juzi Desemba 24,2021.

Kwa mujibu wa ndugu huyo, mtoto mwingine wa marehemu Patricia Mmasi (19) anayesoma nchini China alipata mashaka akiwa China wakati alipojaribu kumpigia simu mama yake lakini haikupokelewa.

Amesema aliamua  kuja Tanzania kwa ajili ya sherehe  za Krisimasi  na alimuuliza  Patrick kuhusu kutoonekaa kwa mama yake na kutopatikana kwenye simu ambapo ndugu yake  huyo  alimjibu kuwa mama yake akitoka huwa hamuagi  na ndipo walipoamua kutoa taarifa polisi.

Amesema polisi walipofika walifanya upekuzi  sehemu mbalimbali za nyumba hiyo ya kisasa ya ghorofa moja na ndipo wakabaini mwili huo ukiwa ndani ya chemba la choo nyuma ya nyumba hiyo na mwili huo umegundulika baada ya siku 14.

Ndugu huyo amedai  marehemu alikuwa akiishi na kijana wake  huyo ambaye ndiye Mmoto wake wa kwanza na mara nyingi walikuwa wakitofautiana .

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamedai mwili huo ulikuwa umeanza kuharibika na umehifadhiwa katika hospital ya Mkoa ya  Mount Meru kwa uchunguzi zaidi.

Kwa mujibu wa ndugu marehemu, mwili wa  Ruth utazikwa nyumbani kwao kesho alasiri katika eneo la Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.