Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Masauni, IGP Wambura waanza safari ya Hanang

Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camilius Wambura  wameanza safari usiku huu kuelekea mkoani Manyara kwa ajili kuungana na vyombo vingine vya ulinzi  na usalama ili  kuongeza juhudi za uokoaji kwa waathirika maporomoko ya tope wilayani Hanang.

Katika msafara huo, Masauni ameambatana pia na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Maduhu Kazi na Kamishna wa Polisi wa Operesheni na Mafunzo, Awadh Haji.

Maporomoko hayo yaliyoua watu 47 na kujeruhi watu 85 yametokea leo Jumapili Desemba 3, 2023 Alfajiri katika maeneo ya Katesh na Gendabi wilayani Hanang mkoani humo.

Maporomoko hayo ya udongo yametokana na mvua zilizoanza kunyesha jana Jumamosi Desemba 2, 2023 saa tatu usiku kuendelea hadi leo asubuhi ilayani Hanang mkoani Manyara.

Maafa hayo yameharibu baadhi ya miundombinu, makazi, maduka na kusimamisha kwa muda shughuli za kijamii na usafiri.

Leo Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Dubai katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28) alitoa salamu za pole huku akisema Serikali itaelekeza nguvu zote wilayani Hanang kwa ajili ya uokozi na kuzuia maafa zaidi.

"Nimeelekeze nguvu zote za Serikali zielekezwe katika uokozi ili kuzuia maafa mengi, imani yangu Serikali ikiwepo basi huduma zote zinazotakiwa zitapatikana niwape pole wananchi, nipo njiani kurudi kushirikiana nao," alisema Rais Samia.