Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Majina 14 ya wanafamilia waliofariki ajalini wakisafirisha msiba

Muktasari:

Majina ya watu 14 wa familia moja waliofariki katika ajali iliyotokea jana Ijumaa usiku wilayani Korogwe mkoani Tanga yametajwa huku wengine 12 wakijeruhiwa.


Korogwe. Majina ya watu 14 wa familia moja waliofariki katika ajali iliyotokea jana Ijumaa usiku wilayani Korogwe mkoani Tanga yametajwa huku wengine 12 wakijeruhiwa.

Idadi hiyo ni miongoni mwa watu 17 waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea katika eneo la Magira Gereza Tarafa ya Mombo wilayani Korogwe, barabara ya Segera - Buiko.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Korogwe, Salma Sued imetaja majina ya wanafamilia hao wakiwamo watoto wawili.

“Waliofariki ni Atanasi Rajabu Mrema, Nestory Atanasi, Augustino Atanasi, Kenned Mrema, Godwin Mrema, Yusuph Saimon, Zawadi Mrema, Elizabeth Mrema, Julieth Mrema, Suzana, Rozina  A Lamosa, Evelina Cosmas Mrema na watoto wawili (mtoto wa binamu na mtoto wa Julieth),” amesema Dk Patrick.

Ajali hiyo imehusisha magari mawili na kusababisha vifo vya watu 17 na majeruhi 12.

Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Mitsubishi Fuso na Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 ikitokea Dar kwenda Moshi kwenye mazishi ambapo chanzo cha ajali hiyo kimetajwa kuwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva Fuso.