Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mabasi ya abiria yagongana, yawaka moto abiria wakiwa ndani Same

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia kwa kuungua moto baada ya basi la abiria kuvaana uso kwa uso na basi dogo na kusababisha kuwaka moto wilayani Same, Mkoa wa Kilimanjaro.
Ajali hiyo imetokea jioni ya leo Jumamosi Juni 28, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni amethibitisha kutokea ajali hiyo.

"Kumetokea ajali, gari dogo la abiria na basi kubwa la abiria yamegongana kisha kuwaka moto, watu wameshindwa kutoka ndani ya hayo magari," amesema Mgeni. 


Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi.