Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kivuko MV Nyerere sasa kipo ufukweni

Muktasari:

  • Kazi ya kukivutia ufukweni kivuko cha Mv Nyerere inaendelea katika mwalo kijiji cha Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe.
  • Kivuko hicho kimesogezwa hadi umbali usiozidi hatua 30 kutoka nchi kavu

 


Ukara. Kivuko cha Mv Nyerere kimevutwa hadi umbali usiozidi hatua 30 kutoka nchi kavu ya ufukwe wa Ziwa Victoria katika kijiji cha Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe.

Kazi ya kukivutia nchi kavu kivuko hicho kilichopinduka Septemba 20, 2018 inafanywa na wataalam wa uokoaji kutoka vikosi vya ulinzi na usalama wakishirikiana na wenzao kutoka makundi mbalimbali.

Wataalam hao wameanza kazi hiyo tangu saa 5:21 asubuhi leo Septemba 28 wakitumia mitambo maalum ya kuvuta vitu vizito.

Ili kisianguke, kivuko hicho kimeegemezwa kwenye meli kubwa ya mizigo ya Mv Nyakibalya inayosindikizana nayo sambamba kuelekea ufukweni.

Soma Zaidi: