Kinana asema hakupenda kuwa katibu mkuu CCM

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. Picha na Mtandao
Muktasari:
Kinana amesema kuwa amekuwa mtendaji wa CCM kwa miaka mitatu na nusu hivyo ni wakati wa kuondoka kama alivyoingia.
Dodoma. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema nafasi hiyo hakuipenda sana lakini kwa kuwa aliombwa na wazee kuchukua nafasi hiyo ya utendaji mkuu wa chama alikuwa hana jinsi.
Kinana amesema kuwa amekuwa mtendaji wa CCM kwa miaka mitatu na nusu hivyo ni wakati wa kuondoka kama alivyoingia.
Alipoulizwa atafanyaje ikiwa ataombwa tena na Rais John Magufuli, amesema atafikiria na kuzungumza naye.
Kwa taarifa zaidi nunua gazeti lako la Mwananchi au soma mtandaoni kupitia www.epaper.mcl.co.tz