Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kilichomkimbiza Dayna kwa Sheddy ni Diamond Platnumz

Msanii Dayna Nyange

Muktasari:

  • Wakati Dayna anatoka kwenye muziki, kazi zake nyingi zilipikwa na mtayarishaji Sheddy Clever ndani ya Studio za Burn Record ambaye alitengeneza wimbo uliomtoa kimataifa Diamond Platinumz, “Number One”.

Dar es Salaam. Nyota wa kike anayetamba na wimbo Chovya, Dayna Nyange anasema aliacha kufanya kazi kwa mtayarishaji Sheddy Clever baada ya kumpa biti yake Diamond Platnumz.

Wakati Dayna anatoka kwenye muziki, kazi zake nyingi zilipikwa na mtayarishaji Sheddy Clever ndani ya Studio za Burn Record ambaye alitengeneza wimbo uliomtoa kimataifa Diamond Platinumz, “Number One”.

Dyna anasema tatizo lilikuwa baada ya Clever kutumia ‘Beat’ yake kutengeneza wimbo wa Number One bila kumshirikisha.

 “Sheddy nimefanya naye kazi kwa muda fulani lakini baada ya kutokea tofauti nikaamua kutafuta mtayarishaji mwingine ambaye ni mtu sahihi, nafanya kazi na T -Touch, anafanya kazi nzuri na  anajua nini anataka, sijafikiria kutoka kwenda sehemu nyingine na siwezi kufanya kazi tena na Sheddy,” anasema.