Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Huduma za zaboreshwa Hospitali ya Katavi

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

Msongamano wa wagonjwa hususani wajawazito wakati wa kujifungua katika Hospitali ya rufaa Katavi umepungua kwa kiasi fulani ikilinganishwa na hapo awali.

Katavi. Ongezeko la miundombinu bora ya kutolea huduma za afya na wataalamu wanaokidhi vigezo  umesaidia kupunguza msongamano wajawazito wakati wa kujifungua  katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi.

Mganga Mfawidhi hospitali hiyo, Yustina  Tizeba akizungumza na Mwananchileo Desemba 7,2021 amesema awali walikabiliwa na changamoto ya msongamano wa wagonjwa hususani wajawazito.

Amesema kwa mwezi mmoja iliwalazimu kuhudumia akina mama wajawazito 500 hadi 600 wakati wa kujifungua  ambapo kwasasa wamepungua na kufikia  180 hadi  200.

“Miundombinu imeongezeka na kuboreshwa,zahanati, vituo vya afya ikiwamo cha Ilembo kinatoa huduma za upasuaji kimetupunguzia sana,” amesema Tizeba akaongeza.

“Tunao madaktari bingwa wanne awali hawakuwapo, Madaktari wa kawaida  walikuwa wanne  kwasasa tunao  15,wauguzi wa degree, wataalamu wa meno na macho hawakuwapo kwasasa tunao,”   

Aidha amesema katika kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wameweka utaratibu wa kutoa huduma za uchunguzi bure ili wananchi  wapime afya zao. 

“Kuanzia Desemba 6 hadi 9, 2021 tutatoa huduma mbalimbali za uchunguzi wa kisukari,shingo ya uzazi,kinywa na meno,macho,presha na mengineyo,”

Hata hivyo zaidi ya wananchi 50 kutoka maeneo tofauti   mkoani  wamejitokeza kupima afya zao wakiomba utaratibu huo uwe endelevu.

“Hii fursa tuliyoipata tunashukru sisi wenye maisha duni kwasababu inatolewa bure,tunaomba waendelee kutoa bure wenye matatizo ni wengi,”wamesema Regna Revocatus  na Francis Watosha.

Mwisho.