Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Hospitali ya Rufaa Mbeya yaboreshwa

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

Wizara Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia ,Wazee na Watoto,kwa kushirikiana na  Mfuko wa Dunia (Global Fund) inatekeleza mradi wa  upanuzi Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Mbeya.  Wizara Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia ,Wazee na Watoto,kwa kushirikiana na  Mfuko wa Dunia (Global Fund) inatekeleza mradi wa  ujenzi wa jengo la  upasuaji  lenye idadi ya vyumba sita , na  wodi  ya wagonjwa yenye uwezo wa  kuchukua  vitanda  89  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza na Mwananchi Leo Jumatano,Desemba 8,2021, Kaimu mganga mkuu wa hosptalin hiyo,Dk Ngwilo Mwakyusa amesema kuwa miradi hiyo imefikia asilimia 78 ya utekelezaji  na  inatarajiwa kukamilika hivi karibuni ili ianze kutoa huduma.

Aidha amefafanua kuwa  kati ya   vitanda 89  katika jengo la upasuaji,  vitanda vya  kawaida ni 72 , vyumba maalumu  10,  huku  vitanda saba  kwa wagonjwa mahututi ambao wako kwenye uangaluzi maalumu. Miradi yote ya jengo la upasuaji  na wodi ina thamani ya Sh 4.469 bilioni .

Dk Mwakyusa amesema kuwa  awali  wizara  kwa kushirikiana na mfuko wa dunia  (Global fund)imetekeleza na kukamilika kwa mradi wa jengo la dharula (EMD)  kwa gharama ya Sh 877.573 milioni.

Dk ,Mwakyusa amesema kuwa uwekezaji wa Serikali  utaboresha huduma za kibingwa za upasuaji katika hospitali  rufaa ya mkoa  na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya Rufaa ya Kanda .

Amesema  katika kutimiza miaka 60 ya Uhuru    Serikali  kwa kutumia mapato ya ndani na kushirikiana na wadau  imekamilisha  miundombinu ya majengo ya  maabara ya kisasa,Jengo la kulaza watoto , wagonjwa wa ndani ,mitambo ya uvunaji wa gesi  , hususan jengo la kuhifadhia maiti  kupitia mpango wa maendeleo ya ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya uviko 19.

Amesema uwekezaji huo umeongeza wigo wa utoaji huduma mbalimbali hususan uwepo wa jengo la dharula la wagonjwa ambapo miaka ilikuwa ni  changamoto kubwa katika utoaji wa huduma  kwa wagonjwa

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Idara ya wagonjwa na nje na Dharula ,Dk ,Abraham Ngonya amesema kuwa wana kila sababu ya kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha ujenzi  wa  jengo la dharura  kwani litakuwa mkombozi mkubwa kwa wagonjwa  wanaofikishwa na kuhitaji msaada wa haraka.

Amesema kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na tayari vifaa vimeshafika ambavyo vinatarajia kufungwa wakati wowote kuanzia sasa na kuanza kupokea wagonjwa na kutoa huduma

Matrida Joseph Mkazi wa Forest mpya  jijini hapa amesema  uwekezaji huo wa Serikali umekuwa kichocheo kikubwa cha upatikanaji wa huduma bora za Afya hususan kwa akinamama wajawazito wanapofika kujifungua  kwa kupata huduma bora na salama.