Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Chalamila apongeza ubunifu wa uongozi wa Tanesco Saccos kuanzisha visa kadi

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

  • Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila atoa kongole kwa uongozi wa Tanesco Saccos kwa kuja na ubunifu wa kuanzisha visa kadi itakayowanufaisha wanachama wao.

Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amezindua kadi ya Visa kwa ajili ya wanachama wa chama cha akiba na mikopo cha Tanesco Saccos, huku akisisitiza umuhimu wa kuwa waadilifu katika utendaji wa kazi zao.

Akizungumza Dar es Salaam jana kwenye uzinduzi wa matumizi ya kadi hiyo yaliyoenda sambamba na mkutano Mkuu wa 55 wa Tanesco Saccos, Chalamila aliwapongeza kwa kuanzisha huduma hiyo ya kadi na kusema kuwa watakuwa katika hadhi ya kimataifa.

"Nadhani nyie ni Saccos ya kwanza kuzindua kadi hii, mnatoka ndani na mnaingia kimataifa niwapongeze sana kwa hilo kwasababu popote unapokuwa hata nje ya nchi mnaweza kuhamisha fedha jambo ambalo ni zuri na hongereni sana,"alisema.

Pamoja na hayo, Chalamila aligusia suala la uadilifu kwa watendaji akisema wengi wanalinganisha na umaskini lakini ni muhimu katika utendaji kazi kuwezesha Saccos kuwa imara.

“Nahimiza umuhimu wa kutumia Saccos yenu kama chanzo cha kuongeza mapato na kubadilisha maisha yenu kiuchumi kwa kufanya vitu vinavyoonekana,”alisema.

Awali, Mwenyekiti wa  Tanesco Saccos, Somoe Nguhwe amesema  ni mkutano  mkuu wa mwaka na tukio  muhimu  la kisheria  lianalowakutanisha viongozi,  watendaji  wa chama  na wawakilishi na kutoa ripoti mbalimbali zinazoonyesha utendaji wa chama kwa mwaka uliopita.

Amesema  kupokea na kujadili  taarifa ya makadrio ya mapato na matumizi  kwa mwaka 2024 na kupitisha maazimio kwa ajili ya utekelezaji kwa mwaka  fedha ujao.

"Mwaka 2022 ulikuwa na changamoto  nyingi  za kiutendaji iliyozalisha matokeo mchanganyiko yakiwemo hasi na chanya katika  utendaji wa shughuli za chama  ikiwemo  changamoto  ya ukwasi katika chama  iliyosababishwa na kuimarika kwa wigo wa kukuopesha kwa wanachama  imepelekea utoaji wa huduma za mikopo kuwa na foleni kusababisha wanachama kutofikia malengo ya mikopo,"amesema.

Alisema Tanesco Saccos idadi ya wanachama imeongezeka kutoka 6,063 mwaka 2021 hadi kufikia 6,354 sawa na asilimia 4.8.

Aidha amesema akiba za wanachama zimekua kutoka Sh41.1 bilioni kwa mwaka 2021 hadi kufikia Sh41.9  bilioni mwaka 2022 na kufanya  ongezeko  la asilimia 5.2 na chama kimetoa faida juu ya akiba na hisa za hiyari kiasi cha Sh1.5 bilioni.

"Jumla ya mkopo yote iliyotolewa katika mwaka 2022 ilifikia Sh57.1 bilioni  ikalinganishwa na mwaka mwaka 2021 ilikuwa Sh48.9 bilioni  sawa na ongezeko la asilimia 16.8," alisema.

Aliongeza kuwa mpango mkakati wa chama kwa kipindi cha miaka mitano mwaka 2024/28 ikiwa ni mpango wa tatu kutekelezwa na chama umejikita kulinda na kukuza mafanikio yote yaliyopatikana katika mipango ya kabla.