Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Lissu, mawakili wake wapinga kesi kusikilizwa kwa njia ya mtandao

Muktasari:

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kwa muda kesi ya kusambaza taarifa za uongo katika mtandao wa Youtube inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu.

Dar es Salaam. Mwenyikiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amegomea kesi yake ya kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya mtandao wa Youtube kusikilizwa kwa njia ya video na badala yake anataka kesi hiyo isikilizwe kwa njia ya wazi.

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi, Aprili 24, 2025 na askari magereza mwenye nyota tatu, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa mara ya pili kusikilizwa kwa njia ya mtandao.

Askari huyo wa Magereza ambaye hakujitambulisha jina lake, ametoa taarifa hiyo kwa njia ya video akiwa mahabusu.

Awali, wakili wa Serikali Mwandamizi, Job Mrema ameieleza Mahakama hiyo kuwa kesi hiyo imeitwa kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa hoja za awali na upande wa mashtaka upo tayari, ila mshtakiwa hayupo mahakama hapo.

Mrema ametoa maelezo hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Geoffrey Mhini.

Kutokana na maelezo hayo, upande wa utetezi umepinga upande wa mashtaka kumsomea hoja za awali mteja wao kwa njia ya video na badala yake wanataka mshtakiwa apelekwe mahakamani kama sheria inavyoelekeza.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala amepinga Lissu kusomewa PH kwa njia ya video kwa madai kuwa sheria iko wazi anatakiwa kuletwa mahakamani.


Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limedhibiti eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam ambako umati wa wanachama na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umefika kufuatilia kesi ya uhaini inayomkabili mwenyekiti wao, Tundu Lissu.


Katika maeneo yote ya mahakama hiyo, polisi wenye silaha, mbwa na farasi wameonekana wakiimarisha ulinzi tangu alfajiri hadi saa tatu wakati kesi hiyo inayosikilizwa kwa njia ya mtandao ilipoanza.

Polisi wakiimalisha ulinzi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Picha na Michael Matemanga


Hadi kufikia saa 3 asubuhi, hakuna kikundi cha watu kilichokuwa kwenye eneo hilo la mahakama na jirani zaidi ya waandishi wa habari ambao wameruhusiwa kusimama umbali wa kama mita 100 kutoka lilipo geti la mahakama.

Polisi wakiimalisha ulinzi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Picha na Michael Matemanga


Polisi hao wametoa amri na kutaka kila mtu aendelee na shughuli zake.


Hata hivyo, waliokwenda kinyume na maagizo hayo wametiwa mbaroni na wengine wakipewa onyo.


Lissu anakabiliwa na kesi mbili, moja ya uhaini na nyingine ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni. 


Kwa mara ya kwanza Lissu alipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo, Aprili 10, 2025. 


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kwa muda kesi ya kusambaza taarifa za uongo katika mtandao wa Youtube inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu.

Kesi hiyo imeahirishwa kwa muda wa dakika 10 kutokana na mtandao kusumbua na kutokusikika vizuri.

Hatua hiyo inatokana na mshtakiwa huyo kutokufikishwa katika mahakama hiyo hivyo, kesi zake mbili zitasikilizwa kwa njia ya video.

Uamuzi huo umetolewa leo, April 24, 2025 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Geoffrey Mhini wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa njia ya video, ili mshtakiwa asomewa hoja za awali.

Hakimu Mhini amesema kutokana na mtandao kusumbua, anaahirisha kwa muda na kama utakuwa bado kuna changamoto atatoa uamuzi.

Hata hivyo, ukumbi huo wa video conference uliopo katika Mahakama hiyo, umejaa hali iliyosababisha baadhi ya watu kuzuiwa kuingia.


Endelea kutembelea mitandao ya kijamii ya Mwananchi