Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Siku 100 za Yas: Ubunifu, tuzo na huduma bora kwa Watanzania

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry Silaa (katikati) akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa chapa ya Yas jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Novemba 6, mwaka jana, Kam­puni ya Mawasiliano Yas (zamani Tigo) ilifanya mabadiliko makub­wa ya chapa zake. Kampuni hii ambayo ilianza kutoa huduma nchini Tanzania miongo mitatu iliyopita kwa jina la Mobitel, ili­badilisha jina lake kuwa Tigo, na sasa jina jipya la Yas linatumika katika mataifa matano ya Afrika ambapo inatoa huduma.

Mbali na kubadilika kwa chapa ya kampuni, pia jina la huduma zake za kifedha kwa njia ya simu za mkononi ambalo awali liliju­likana kama Tigo Pesa, ilibadi­lika na kuwa Mixx by Yas. Huu ni mchakato wa kawaida katika biashara lakini una umuhimu mkubwa katika maendeleo ya kampuni na biashara kwa ujumla.

Katika uzinduzi wa jina hili jipya, uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya mawasiliano, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa alielezea mabadiliko haya kama hatua muhimu kuelekea ujumuishwa­ji wa kifedha na kidijitali kwa Watanzania.

Afisa Mkuu wa Biashara wa Yas, Isack Nchunda akizungumza kuhusu mafanikio ya siku 100 za chapa za Yas na Mixx by Yas tangu kufanyika kwa mabadiliko ya chapa hizo.

Mabadiliko haya ni sehemu ya dhamira ya kampuni ya Axian Telecom Group ambayo ni kam­puni mama ya Yas. Mabadiliko haya sio tu yamefanyika Tan­zania, bali ni mpango wa Axian Telecom Group kuhakikisha kam­puni zake tanzu kote Afrika zina jina moja lenye nguvu na linalo­endana na maono ya kampuni.

Kwa Yas, mabadiliko haya yana­onyesha dhamira ya kampuni ya kuleta mabadiliko ya kisasa kati­ka sekta ya kidijitali na kifedha. Ni njia ya kuimarisha biashara na kuongeza wigo wa huduma kwa wateja. Ingawa kuna changamo­to zinazohusiana na mabadiliko haya, manufaa yake ni mengi na yanachangia ukuaji wa biashara na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Katika siku 100 tangu Yas na Mixx by Yas kubadilisha chapa kutoka Tigo na Tigo Pesa, tume­shuhudia mageuzi makubwa kati­ka sekta ya mawasiliano. Kam­puni ya Yas imelenga kuwaweze­sha Watanzania kunufaika na fursa za kidijitali na za kifedha zilizopo hapa Tanzania.

Akizungumzia siku 100 za Yas, Afisa Mkuu wa Biashara wa Yas, Isaac Nchunda anasema kuwa katika kipindi hiki cha siku 100 za kwanza tangu kufanya maba­diliko ya chapa, kimekuwa kipin­di cha mafanikio makubwa kwa wateja na washirika wa Yas na Mixx.

“Yas na Mixx ni kampuni yenye lengo la kumuwezesha kila Mtan­zania kunufaika na fursa za kidi­jitali. Vile vile, tunataka kutam­bulika kama wabia kwa kila mdau wetu,” anasema Nchunda.

Anasema: “Mimi kama Afisa Mkuu wa Biashara, kila nikiamka ninawaza ni jinsi gani tunaweze­sha Watanzania kunufaika na fursa zilizopo kwenye ulimwengu wa kidijitali popote walipo. Hilo ndio lengo letu kama chapa, hayo ndio maono yetu.”

Anaongeza kuwa: “Katika siku 100 za Yas na Mixx, tunatambua kuwa tusingefanikiwa kwa kiasi tulichofanikiwa bila wateja wetu na wadau mbalimbali wa sekta ya mawasiliano ambao wameku­wa nasi kuanzia siku ya kwanza tulivyozitambulisha chapa zetu za Yas na Mixx.”

Mafanikio ya siku 100

Mafanikio ya siku 100 za Yas ni pamoja na kubadilisha maisha ya Watanzania zaidi ya 1,300 kupitia promosheni ya Magift ya Kugift ambapo, wateja na washirika wa kibiashara wamepatiwa zawadi zenye thamani mbalimbali.

“Tumetoa magari mawi­li mapya aina ya KIA Sorento ambayo hayajatumika kabisa (kilomita sifuri), zaidi ya Sh 840 milioni zimetolewa kwa wateja na washirika wetu huku simu jan­ja zaidi ya 540 zikinyakuliwa na washindi mbalimbali,” anasema Nchunda.

Hii ni sehemu ya dhamira ya dhati ya Yas ya kuwashukuru wateja wake na kuendelea kuwa­pa thamani zaidi kupitia huduma bora na promosheni za kipekee.

Yas imewekeza kwenye tekno­lojia za kisasa zinazowezesha upatikanaji wa mtandao wenye ubora na wa kasi zaidi. Vile vile, imeboresha huduma zake za Mixx kwa ujumla ili kuhakikisha kuwa huduma za kifedha zinapatikana wakati wowote bila kujali maeneo mteja alipo.

Lengo ni kuwawezesha Watan­zania kutumia fursa za kidijitali kwa urahisi zaidi iwe kwa mteja mmoja mmoja au makampuni/biashara.

Tuzo kedekede

Katika kipindi kifupi cha siku 100, Yas imeendelea kuthibitisha ubora wake kwa kushinda tuzo mbalimbali za kitaifa na kimatai­fa.

YAS imenyakua tuzo ya Mtan­dao Wenye Kasi Zaidi Tanza­nia kwa miaka miwili mfululizo kutoka kampuni ya Kimataifa ya Ookla. Ripoti za robo mwaka za Mamlaka ya Mawasiliano Tanza­nia (TCRA) zimeitaja Yas kuwa Mtandao Bora mara tatu mfulu­lizo.

Pia, katika vipindi tofauti, kam­puni hiyo imetajwa kama Mtoa Huduma Bora wa Intaneti Tan­zania, Kampuni Yenye Teknolo­jia Endelevu za Tehama zenye Ufanisi wa Nishati, Mshindi wa Pili – Matumizi Bora ya Tehama kwenye Elimu (eShools Project), Mshindi wa Kwanza – Mlipaji Kodi Mkubwa wa mwaka (Ush­uru wa Forodha) na Mshindi wa Kwanza – Kampuni inayozingatia misingi na kanuni bora za Uku­sanyaji wa Ushuru wa Forodha.

Tuzo hizi zinadhihirisha dhamira yake ya kuwa kinara wa sekta ya mawasiliano Tan­zania kwa ubora wa huduma na mchango katika maendeleo ya Taifa.

Ushirikiano wa kimkakati kufiki­sha huduma za kibunifu popote Tanzania

Katika siku hizi 100 za mwanzo, Yas imeingia kwenye makubalia­no ya kimkakati ili kufikisha hudu­ma za kibunifu kwa Watanzania kwa kushirikiana na Kampuni ya ITHUBA ambao ni waendeshaji rasmi wa jukwaa la Bahati Nasibu ya Taifa.

“Ushirikiano wetu umejikita kwenye kutumia teknolojia ya kisasa kuhakikisha kuwa Watan­zania wanafurahia michezo ya kubahatisha popote pale walipo.”

“Tumeshirikiana na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ili kuwezesha Watanzania kushiriki moja kwa moja kwenye uwekezaji kwa kutumia teknolojia iliyorahi­sishwa na yenye usalama zaidi,” anasema Nchunda.

Hitimisho

Katika siku 100 za kwanza, Yas imeleta mabadiliko makub­wa kwa wateja wake, imeimar­isha huduma zake, imejizolea tuzo muhimu zinazothibitisha kuwa wao ni vinara wa sekta ya mawasiliano, na inashirikiana na wadau wa sekta mbalimbali kuhakikisha kuwa teknolojia ina­tumika ipasavyo kurahisisha upa­tikanaji wa huduma mbalimbali hapa Tanzania.

“Huu ni mwanzo tu – tunaahi­di kuendelea kuboresha huduma zetu ili kuzidi matarajio ya wateja kila siku kwa sababu huu ni waka­ti wetu,” anahitimisha Nchunda.