Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ripoti ya kampuni ya Carbon Tanzania yaonyesha maendeleo makubwa katika jamii kutokana na faida za miradi ya hewa ukaa

Zahanati ya Mpembe iliyopo katika Milima ya Ntakata.

Muktasari:

  • TSh 9.4 Bilioni (Dola za Marekani 3.7Millioni) zimepokelewa na jamii na vijiji vilivyoko kwenye miradi kwa mwaka 2024.
  • REFLECT for Nature’, yafanya tathmini ya faida ya miradi na kugundua manufaa makubwa kwa jamii
  • Mradi wa Makame Savannah waonyesha faida mara kumi zaidi kwenye kila uwekezaji uliofanyika

Juni 23, 2025 Carbon Tanzania ilizindua ripoti yake ya mwaka 2024, ikionyesha faida kubwa kwenye miradi yake ya kulinda misitu kwa jamii, bioanuwai na mazingira nchini. Lengo kuu la ripoti hii ni kuelezea jukumu muhimu la Ufuatiliaji, Kuripoti na Uthibitishaji (MRV) wa kijamii katika kuelewa na kuimarisha manufaa ya utunzaji wa misitu na mazingira kwa ulimwengu na jamii.

Ripoti hii inasisitiza dhamira ya Carbon Tanzania ya "kusikiliza kwa ukaribu zaidi na kujifunza kutoka kwa washirika wetu mira­dini." Hili limefaniikiwa kupitia mbinu bunifu ya REFLECT for Nature (RfN) ya tathmini ya faida za kijamii, ambayo inakusanya mitazamo ya jamii kuhusu jinsi mapato ya hewa ukaa yanavyon­ufaisha maisha yao na uhusiano na misitu wanayoilinda.

"Falsafa yetu kuu haijabadilika: watu ndio kiini hasa cha hadithi hii ya uhifadhi," wanasema Marc na Jo, Waanzilishi Wenza wa Car­bon Tanzania. "Ripoti ya mwaka 2024, hususani kupitia kufanya kazi na REFLECT for Nature, imetuwezesha kufahamu maba­diliko makubwa ambayo yanaele­za faida na kuhakikisha kuwa hatusababishi madhara huku tukijenga ubia wenye usawa."


Matokeo ya ripoti ya mwaka 2024 yaonyesha manufaa makubwa kwa jamii

Utoaji wa fedha: Carbon Tan­zania imeelekeza zaidi ya Sh 9.4 bilioni (Dola za Marekani 3.7M) kwenda kwenye baadhi ya jamii kwa mwaka 2024. Fedha hizi zimesaidia kuboresha huduma muhimu za kijamii kama afya, elimu na miundombinu huku manufaa mengine yakionekana katika ulinzi wa wanyamapori na mazingira.

Shule ya Msingi Makame iliyopo eneo la Makame Savannah.

Mabadiliko yanayoongozwa na jamii katika eneo la Makame: Tath­mini iliyofanywa na REFLECT for Nature katika mradi wa Makame Savannah ulionyesha uwiano thabiti wa kijamii, kiutawala na maono ya pamoja. Tathmini hii ikiongozwa na jamii yenyewe, wamegundua mradi huu unaleta mabadiliko makubwa, ukikadiri­wa kurudisha thamani ya kijamii mara 10 zaidi (1:10), na thamani kamili ya kijamii ikiwa Dola za Kimarekani 6,727,659 kupatikana, kulingana na tathmini za mwaka 2024 zilizofanywa kwa kushiriki­sha jamii husika kulingana na kia­si cha fedha zilizopatikana.

Ikiwa Elimu ni kipaumbele: Katika eneo la Makame, asilimia 94 ya jamii wanathamini sana elimu ya watoto wao na hivyo, kuweka kipaumbele kwenye mapato yatokanayo na hewa ukaa katika ujenzi wa madarasa na mabweni, pamoja na ufadhi­li kwa wanafunzi hadi elimu ya juu. Katika miradi yote, ada za wanafunzi 72 wa vyuo vikuu zil­ilipwa, na watoto 9,840 wa eneo la Makame sasa wanafaidika na upatikanaji bora wa elimu kupitia miundombinu mipya na ufadhili.

Kuimarisha usalama wa ardhi na kupunguza mzigo wa kiuchumi: Ripoti ya mwaka 2024 inathibit­isha jinsi jamii zinavyoweka ulinzi mathubuti unaotokana na uwezeshwaji kutoka kwenye fed­ha zitokanazo na mapato ya mra­di kwenye maeneo yao. Wanaki­jiji wanaweza kuripoti shughuli zinazotiliwa shaka kwa walinzi wa uhifadhi (VGS), ambao wana­fanya doria katika maeneo yaliyo­hifadhiwa ili kupunguza uvamizi na ujangili. Hii imeboresha mal­isho ya mifugo na hivyo kupun­guza kwa kiasi kikubwa gharama kwa wananchi wengi wa jamii za Kimasai.

Kuwezesha wanawake: Mika­kati ya uwezeshaji wanawake inapewa kipaumbele kikubwa, huku wanawake 64 wakifanya kazi kama walinzi wa uhifadhi; takriban asilimia 20 ya walinzi wote (VGS). Pia wanawake 183 wakiwa wanachama wa benki ya jamii ya uhifadhi (COCOBA) kati­ka mradi wa Milima ya Ntaka­ta, inayojumuisha asilimia 53 ya wanachama wote wa COCOBA.

Tathmini iliyofanywa kwenye mradi wa Makame umeonyesha kuwepo kwa viwango sawa vya umiliki wa mali kati ya wanawake na wanaume, jambo linalosaidia kupunguza changamoto za kijin­sia na kuleta maendeleo chanya katika harakati za kupigania usa­wa wa kijinsia.

Uwazi na uwajibikaji: Katika eneo la Makame, asilimia 82 ya wanajamii waliohojiwa wamese­ma kuwa mradi wa hewa ukaa unasimamiwa kwa uwazi. Carbon Tanzania inatumia kikamilifu taarifa ya RfN kutoka eneo la Eya­si (mradi wa Yaeda-Eyasi), ija­pokuwa asilimia 64 ya wanajamii walieleza kutokushirikishwa katika kufanya maamuzi kwenye mchakato wa kuboresha taratibu za ushiriki na ushirikishwaji.

Ajira na ukuaji wa uchumi: Utekelezaji wa mradi uliweze­sha kutoa ajira kwa watu 448, wakiwemo VGS 325 (ongezeko la asilimia 15 kutoka mwaka 2023) na mabalozi 96 wa hewa ukaa (ongezeko la asilimia 533). Vikun­di vya COCOBA, vikichochewa na fedha za hewa ukaa, vimetoa mikopo midogo iliyosaidia kuku­za uchumi na kuboresha maisha, ikiwa ni pamoja na kuboresha makazi, ikiwemo kuhama kutoka nyumba za nyasi hadi za matofali.

Ngo’mbe dume wapya kwa ajili ya wafugaji wa eneo la Makame Savannah.

Dhamira ya Carbon Tanzania katika kuandaa na kutekeleza miradi yake inaenda mbali zaidi hadi kutumia vigezo vya uthibit­isho na uhakiki chini ya taasisi ya kimataifa ya Verra, VM0048, ambayo imekidhi vigezo na Kanuni za Msingi vya Hewa Ukaa (CCP) na Baraza la Uadilifu la Soko la Hiari la Hewa Ukaa (ICVCM). Matumizi ya vigezo hivi yameimarisha uadilifu, uwazi na imani ya soko na hivyo kuhakiki­sha kwamba viumbe hai na jamii zinaendelea kunufaika na mira­di hiyo chini ya viwango vina­vyotambulika kimataifa.

Ripoti ya mwaka 2024 ni uth­ibitisho wa kweli kwamba jamii inapopewa mamlaka na haki mili­ki ya ardhi yao na kushiriki kika­milifu katika usimamizi na manu­faa ya kifedha ya uhifadhi wa mis­itu, huleta maboresho makubwa na yanayopimika katika maisha yao, maendeleo, na kuboresha mifumo ya ikolojia wanayoilinda.

Ushirikiano na wadau, Serikali pamoja na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs)

Carbon Tanzania inatambua umuhimu wa ushirikiano kati­ka kufikia malengo ya uhifadhi endelevu. Kampuni imejenga mahusiano thabiti na mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na masuala ya uhifadhi nchini na kimataifa. Ush­irikiano huu unajumuisha kuba­dilishana utaalamu, kushirikiana katika utafiti na ufuatiliaji, na kuunganisha nguvu katika ute­kelezaji wa miradi.

Kwa kufanya kazi kwa kushirik­iana na Serikali pamoja na taas­isi zisizo za kiserikali kama vile Honeyguide, Community Wild­life Management Area Consortia (CWMAC), World Wide Fund for Nature (WWF), The Nature Con­servancy (TNC), Wildlife Man­agement Areas (WMAs), Uja­maa Community Resource Team (UCRT) na halmashauri za wilaya, Carbon Tanzania inaweza kufikia maeneo makubwa zaidi, kuonge­za ufanisi wa programu zake, na kuhakikisha kwamba juhudi za uhifadhi zinakuwa na matokeo makubwa na ya kudumu kwa jamii na mazingira.

Kuhusu Carbon Tanzania

Carbon Tanzania ni kampuni ya kitanzania ambayo inachan­gia katika kukuza uchumi wa nchi na watu wake kwa kutunza mis­itu asili na viumbe hai kupitia uuzaji wa vyeti vya hewa ukaa iliyookolewa na kuwawezesha watanzania kupata mapato kuto­kana na uhifadhi wa mazingira yao.

Vyeti hivi hununuliwa na mashirika mbali mbali ndani ya nchi pamoja na kimataifa yenye malengo na mikakati chanya ya kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kwa kuwekeza katika shu­ghuli za uhifadhi zinazochochea na kuleta matokeo bora katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, jamii na wanyamapori nchini.