Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

GGML: Kinara wa maendeleo endelevu ya mazingira Tanzania

Diwani wa Viti Maalumu wa Kata ya Kasamwa, Diana Magayane (aliyeketi katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na mwakilishi kutoka GGML pamoja na wanafunzi na walimu wa Shule ya Sekondari Kasamwa wakati wa mdahalo wa shule ulioandaliwa na GGML kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani.

Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2025 chini ya kaulimbiu “Tuwajibike Sasa; Dhibiti Matumizi ya Plastiki,” Kampuni ya Geita Gold Mine Limited (GGML), ambayo ni kampuni tanzu ya AngloGold Ashanti, inathibiti­sha upya dhamira yake madhubuti ya kulinda mazingira, kusimamia miradi uendelevu na uchimbaji madini usioharibu mazingira hapa Tanzania.

Wakati huu ambao dunia ina­sisitiza kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kulin­da mazingira, GGML inaonyesha mfano bora wa jinsi uchimbaji wa kisasa wa madini unavyowe­za kuyatunza mazingira badala ya kuyaharibu.


Kampuni ya madini inayolinda mazingira

Siku ya Mazingira Duniani ni wito wa kimataifa wa kulinda dun­ia tunayoishi. Kwa GGML, kaulim­biu ya mwaka huu ina maana kubwa.

Diwani wa Viti Maalumu wa Kata ya Kasamwa, Diana Magayane, akipanda mti katika Shule ya Sekondari Kasamwa wakati wa mdahalo wa shule ulioandaliwa na GGML kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani.


Tunaliangalia jambo hili kama fursa muhimu. Matumizi ya plastiki ni changamoto iliyo wazi, lakini pia ni nafasi ya kuchukua hatua. Tumejikita katika misingi ya uchumi endelevu ambao unalenga kupunguza taka, kurejesha taka kuwa malighafi mpya zinazoweza kutumika tena, na kusaidia jamii kuwa safi na endelevu.”


Kupambana na changamoto zilizopo za mazingira

GGML inafanya kazi katika Mkoa wa Geita, ambako inakabiliana na changamoto za kimazingira amba­zo kampuni nyingi za madini huz­iepuka.

Kampuni hiyo inakabiliana na ukataji miti ovyo unaosababish­wa na shughuli za kibinadamu; uchafuzi wa mazingira unaotoka­na na shughuli za uchimbaji madi­ni na taka za mijini; inapunguza matumizi ya plastiki zinazotumi­ka mara moja kwa kushirikiana na wadau wa ndani; inalinda vyanzo vya maji vya asili na kuhamasisha uhifadhi wake na kusaidia jamii na kukabiliana na mabadiliko ya tabi­anchi kupitia programu za upan­daji miti na uelimishaji. Haya ni sehemu ya mkakati wa kisayansi uliojikita kusaidia jamii.


Upandaji miti

Mojawapo ya miradi yenye mchango mkubwa ya GGML ni mradi wa kupanda miti, ambapo maelfu ya miti asilia hupandwa kila mwaka. Hili huambatana na urejeshaji wa ardhi katika mae­neo yaliyochimbwa, ambako miti na uoto wa asili hurudishwa kwa lengo la kuhuisha tena viumbe hai na kuzuia mmomonyoko wa ardhi.

Maji pia ni kipaumbele kikubwa. GGML imewekeza katika mitambo ya kisasa ya kutibu maji macha­fu, kuhakikisha maji yanayorudi kwenye mazingira kutoka migodi­ni yanakidhi viwango vya Tanzania na vya kimataifa.

Mbali na hayo, mgodi ume­punguza utegemezi wa vyanzo vya maji safi kwa kuchakata na kutumia tena maji kutoka kwenye mabwawa ya akiba ya matope ya machimbo (Tailings Storage Facil­ity – TSF).

Na mambo haya hayaishii hapo. Vifaa vya kutenganisha taka vimewekwa katika mgodi na mae­neo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa Geita ili kusaidia usi­mamizi bora wa taka, hususan plastiki. Kujitoa huku kumeifanya GGML kuwa kampuni kinara katika mapambano dhidi ya uchafuzi wa mazingira.


Ubunifu na miradi endelevu

Ili kupunguza athari kwenye mazingira, GGML imeamua kujik­ita kwenye ubunifu. Mgodi sasa umeunganishwa na gridi ya Tai­fa ya umeme wa Tanzania, jambo lililopunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya majenereta ya dizeli na hivyo kupunguza hewa ya ukaa.

Aidha, GGML inatumia mifumo ya kidijitali kufuatilia uchafuzi wa hewa, maji, na kelele, kitu kin­achowezesha hatua za haraka na uboreshaji wa mara kwa mara.

Mwanafunzi akitoa maoni wakati wa mdahalo wa mashule ulioandaliwa na GGML kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani.

Eneo jingine lililofanyiwa mageuzi ni udhibiti wa taka kwa njia ya kidijitali, hususan plasti­ki na taka hatarishi. Hii huonge­za uwazi na kuruhusu kampuni kuboresha mbinu zake za usima­mizi wa taka, hivyo kupunguza hatari kwa watu na mazingira.


Uwekezaji katika jamii

Miradi endelevu ya mazingira ya GGML haishii ndani ya mgodi pekee. Kampuni inaamini kwamba mabadiliko ya kweli huanzia kwa watu, hivyo imewekeza sana kati­ka kuelimisha jamii.

Shule, vikundi vya wanawake, na vyama vya vija­na hushirikishwa katika mafunzo kuhusu mabadiliko ya tabianchi, usimamizi wa taka, na uhifadhi wa mazingira.

Mfano mzuri ni Mradi wa Vitalu vya Miti ya Kupandwa, ambapo wanajamii huwezeshwa kukuza miche ya miti inayotumika baa­daye kurejesha maeneo yaliyo­haribiwa na uchimbaji madini.

Huu ni ushindi kwa pande zote mbili ambapo vijana hupata huwezesh­wa kiuchumi kupitia ajira zin­azohusisha utunzaji mazingira na kujenga mazingira yenye afya ya mifumo ya ikolojia kwa vizazi vijavyo.

Jamii zinazopitiwa na bomba la maji kutoka Ziwa Victoria pia zin­anufaika na upatikanaji wa maji safi, kupitia uwekezaji wa GGML katika miundombinu endelevu ya maji.

Katika maeneo ya vijijini, pro­gramu za kilimo endelevu na kili­mo cha miti zinasaidia wakulima kuongeza mavuno huku wakilinda udongo na kupunguza uharibifu wa mazingira.


Safari ya kujifunza, kujitoa

Licha ya changamoto zilizopo kwenye safari ya GGML kwenye ajenda ya mazingira, kampuni imetambua kwamba ushirikishwa­ji wa jamii mapema huleta mafani­kio, na kwamba maamuzi yanapaswa kuongozwa na sayansi na taar­ifa (data).

Pia, imejifunza kwamba ushirikiano na Serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na taasisi za elimu ni muhimu kwa matokeo ya muda mrefu.

Tunapoangalia mbele zaidi, GGML haikusudii kushusha mapanga chini kwenye mapam­bano haya. Tumejipanga kufikia lengo la kimataifa la AngloGold Ashanti la utoaji sifuri wa hewa ya ukaa, kuongeza uwekezaji kati­ka teknolojia rafiki kwa mazingi­ra, kupanua mipango ya kuhifadhi bioanuwai, na kutekeleza mpan­go wa utunzaji wa maji unaolinda rasilimali hii adhimu,” anasema Dk Kiva Mvungi, Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira wa GGML.


Wito

Kuelekea katika Siku hii ya Mazingira Duniani, GGML ina­toa ujumbe wa wazi na muhimu: Dunia haitaki ahadi zaidi, inahi­taji maendeleo halisi. Kampuni inawaalika wadau wote, makam­puni, jamii, na wananchi, kuchukua hatua muhimu kumaliza uchafuzi wa plastiki na kulinda mazingira yetu ya pamoja.

Tanzania inapoendelea na safari yake ya maendeleo, GGML inabaki kuwa kampuni mfano wa uchim­baji wa madini wenye dhamira ya dhati ambapo ukuaji wa uchumi, ulinzi wa mazingira, na ustawi wa jamii huenda pamoja.