Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo mawaziri, William Lukuvi (Sera, Bunge na Uratibu) na Innocent Bashungwa (Mambo ya Ndani) wakishiriki Ibada ya kumwombea aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, hayati John Magufuli.
Dk Magufuli alifariki dunia Jumatano ya Machi 17, 2025 katika Hospitali ya Mzena, Kijitonyoma jijini Dar es Salaam. Leo Jumatatu, Machi 17, 2025 imetimia miaka minne tangu kifo chake.
Waombolezaji hao wamejitokeza kwa wingi katika Parokia ya Mtakatifu Yohana Muzeyi Chato, Mkoa wa Geita inakofanyika Ibada hiyo kuungana na wanafamilia akiwemo mjane wa Magufuli, Mama Janeth.
Ibada hiyo inaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge- Ngara, Severine Niwemugizi.