Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Sudan wachekelea kupewa sapoti Zanzibar 

Dar es Salaam. Kocha wa timu ya taifa la Sudan, Kwesi Appiah, amesema timu yake ipo tayari kukabiliana na changamoto ya robo fainali ya mashindano ya CHAN 2024 dhidi ya Algeria ambao ni wanafainali za mwaka 2022.

Sudan ilimaliza nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa kundi D ikiwa na pointi tano sawa na Senegal huku Algeria yenyewe ikishika nafasi ya kundi C ikiwa na pointi sita nyuma ya Uganda.

“Kuendelea katika hatua za mwisho kunamaanisha michezo migumu zaidi. Mechi ya Senegal ipo nyuma yetu, sasa tunafikiria mchezo dhidi ya Algeria. Haitakuwa rahisi, lakini tutawapa changamoto kubwa,” alisema.

Akiwa na kujiamini kwa hali ya juu, rekodi isiyopoteza, na mwendo wa ushindani unaojenga, Sudan inaingia kwenye hatua za kuondoa ikiwa mojawapo ya timu za kushangaza za mashindano.

Licha ya kikosi cha Sudan kufanya maandalizi siku nne tu kabla ya mashindano hayo kuanza, imekuwa moja ya timu ambazo zimeshangaza wengi hasa baada ya kuichapa Nigeria mabao 4-0 katika hatua ya makundi huku ikitoa sare dhidi ya bingwa mtetezi, Senegal.

Akiongelea sapoti ambayo Sudan inaipata Zanzibar ambako walicheza mechi zao za makundi na pia watacheza robo hapo kesho, Jumamosi dhidi ya Algeria kocha huyo alisema; "Watu wa Zanzibar wanafanana na Waasudani. Wanasema Kiarabu, hivyo kulikuwa na uhusiano wa mara moja tulipoingia."

Katika mechi tano zilizopita kati ya timu hizi mbili katika mashindano yote ikiwemo pia mechi za kirafiki, Algeria imekuwa na matokeo chanya zaidi dhidi ya Sudan, ikifunga jumla ya mabao 7-0 katika michezo miwili ya hivi karibuni ya mwaka 2021 na 2022.

Hata hivyo, Sudan inarekodi nzuri katika mashindano ya CHAN dhidi ya timu hiyo kwani Februari 2011 iliibuka na ushindi wa bao 1-0.