Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Polisi yawaonya wanasiasa uchaguzi wa kesho

Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya 

Muktasari:

Uchaguzi wa udiwani katika kata 77 na jimbo la Buyungu, Kakonko utafanyika kesho nchini.


Mtwara. Jeshi la polisi mkoani Mtwara limewaonya wanasiasa  wanaofanya mikusanyiko isiyo  halali kwa madai ya kulinda kura katika uchaguzi mdogo unaotegemewa kufanyika kesho Jumapili.

Uchaguzi wa udiwani katika kata 77 na jimbo la Buyungu, Kakonko utafanyika kesho nchini.

Akizungumza leo Agosti 8 Kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya amesema jeshi hilo limejipanga na lina askari wa kutosha kutuliza ghasia.

 Amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya kidemokrasia na kumchagua kiongozi wanayemtaka.

“Tunazo taarifa baadhi ya vyama vya siasa wamejipanga kufanya mikusanyiko isiyo halali katika vituo vya kupiga kura kwa kile wenyewe wanachokiita kulinda kura zao zisiibiwe, tunawakumbusha kazi ya kulinda usalama wa raia na mali zao ni jukumu la jeshi la polisi na sio mtu mwingine,” amesema

Amesema hata kazi ya kulinda wananchi wakati wakipiga kura ni kazi ya jeshi  hilo na si vinginevyo.

Pia amewaomba wananchi kurudi nyumbani mara baada ya  kumaliza kupiga kura  na  waendeleze utulivu wakisubiri matokeo.

“Tutatakuwa na askari wengi sana katika vituo vyote vinavyotarajiwa kupigwa kura, kwa hiyo mtu yeyote asijipe jukumu hilo, hivyo vyama vinavyojipanga  kutekeleza jukumu la polisi hatujaomba msaada sisi,” amesema

Amesema polisi wana askari wa kutosha kuweza kusimamia uchaguzi.

 Uchaguzi wa madiwani  Mtwara, utafanyika katika kata tatu za Makonga, Nanguruwe na Nalingu.