Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Padri Mbahulira afariki dunia

Bukoba. Padri Ireneus Mbahulira (80) wa jimbo Katoliki Bukoba amefariki dunia katika hospitali ya Mugana wilaya ya Misenyi akipatiwa matibabu.

Akizungumza jana Jumamosi Januari 23, 2021 Askofu msaidizi wa jimbo hilo,  Methodius Kilaini ameieleza  Mwananchi Digital  kuwa kifo cha  Mbahulira kimetokea Januari 22, 2021 katika hospitali ya Mugana Wilaya ya Misenyi alikokuwa amelazwa wiki moja iliyopita.

Amesema katika matibabu mbali na kuwekewa dripu kadhaa,  padri huyo aliwekewa mashine za kumsaidia kupumua.

Amesema padri huyo alizaliwa mwaka 1942 na mwaka 1969 alipata daraja la upadri  na alihudumu  kama paroko Jimbo la Bukoba Parokia ya Buyango Wilaya ya Misenyi.

"Mwaka 2018 aliamua kurudi nyumbani ambapo alipangiwa Parokia ya Rukindo wilaya ya Muleba baadaye alihamishiwa Minziro wilaya ya Misenyi, " amesema Kilaini

Amesema mazishi yatafanyika Jumatatu Januari 25, 2021.