Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mwanafunzi kidato cha kwanza abakwa hadi kufa

Muktasari:

  • Watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kwa  tuhuma za kubaka hadi kufa mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Mkwasa.

Hai. Watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kwa  tuhuma za kubaka hadi kufa mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Mkwasa.

Akizungumza leo Jumatatu Juni 28, 2021 Kamanda wa Polisi mkoani humo, Amon Kakwale, amesema tukio hilo limetokea jana Jumapili Juni 27, 2021 katika kijiji cha Mungushi Kati  Wilaya ya Hai.

Amemtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Sayuni Ruben (14), “huyu  binti alikutwa amefariki baada ya watuhumiwa kuutupa mwili wake baada ya kumbaka.”

Amesema Juni 26, 2021 binti huyo aliondoka nyumbani kwao na kwenda katika  kanisa la Lutherani Mungushi kwa ajili ya maandalizi ya sherehe ya vijana.

Amesema wakati mwanafunzi huyo anarudi nyumbani  saa 1:30 usiku alikutana  na watu hao waliombaka.