Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mvua Siha zaleta msiba, mwili wa mwanamke wapatikana

Muktasari:

  • Mwanamke huyo pamoja na mwenzake wanadaiwa kupotea November 22, 2023 wakidaiwa  kuchukuliwa na maji ya Mto Biriri, wakati wakitokea Soko la Makiwaru kununua mahitaji ya nyumbani.

Siha. Wananchi wa Kata Songu Kijiji cha Ndumbaru, wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro wamefanikiwa kupata moja ya miili ya wanawake wawili wanaosadikiwa  kusombwa  na maji kutokana na mvua kubwa zinazonyesha wilayani hapa.

 Wanawake hao Eliakesia Akyoo (61) na Eliakesia Elisante (55) wanadaiwa kupotea November 22, 2023 kwa madai ya kusombwa  na maji ya Mto Biriri, wakati wakitokea Soko la Makiwaru kununua mahitaji ya nyumbani.

Mkuu wa Wilaya ya Siha, Christopher Timbuka amethibisha kutokea kwa jambo hilo na mmoja wa wanawake hao  amepatika na wanaendelea kumtafuta mwingine.

Aidha, DC Timbuka amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ikiwamo kuchimba mitaro hasa kwenye nyumba zilizozingirwa na maji ili kuyapa njia ya  kupita.

Akizungumza na waandishi wa habari kijijini hapo, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Issaya Mkilindi amesema kuwa wanaendelea na shughuli ya kumtafuta mama huto wakipita  pembezoni mwa mto huo na maeneo mengine.

“Siku ya Jumatano, wanawake hao walikwenda Soko la Makiwaru kwa ajili ya kupata mahitaji, lakini wakati wanarejea makwao, hatujui nini kimewapata lakini tunahisi kutokana na mvua kuendelea kunyesha, walikuta mto umefurika maji hivyo kusabisha kubebwa na maji,” amesema na kuongeza;

“Mmoja wa wakina mama hao ilikuwa afanye ubarikio wa mtoto wake jana Novemba 24,2023. Tunaendelea kumtafuta,”amesema Mkilindi.