Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Madaktari bingwa 35 kutoa matibabu bure Mbeya

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Rodrick Mpogolo akizungumza na madaktari bingwa na bobezi baada ya kuwasili na kupangwa kwenye Hosptali za Wilaya saba mkoani hapa. Picha na Hawa Mathias

Muktasari:

  • Madaktari bingwa na bobezi wameweka kambi ya siku tano Mbeya kwa lengo la kutoa huduma za  matibabu ya kibigwa bure kwa wananchi kupitia programu ya ‘madaktari bingwa wa Rais Samia tumekufikia’

Mbeya.  Timu ya madaktari bingwa  35 imewea  kambi ya siku tano jijini hapa kwa ajili   ya kutoa huduma  bure za  uchunguzi na matibabu ya  kibingwa kwa wananchi.

Kambi hiyo imeanza leo Jumatatu Mei 13, 2024 itadumu hadi Mei 17 mwaka huu  na itahusisha  hospitali zote za wilaya zilizopo katika halmashauri saba za Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kambi hiyo Katibu Tawala Mkoa, Rodrick Mpogolo amesema wamewapokea madakrari 35 na kila  halmashauri watapelekwa madaktari bingwa watano.

Miongoni mwa huduma za uchunguzi na  matibabu yatakayotolewa  ni  ya wanawake, wajawazito, watoto njiti, dawa za usingizi, ganzi, upasuaji wakiwepo wagonjwa wa ndani na nje.

Amesema  lengo la Serikali kusogeza huduma kwa wananchi ni kutaka waondokane na  changamoto za kutembea umbali mrefu.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Elizabeth Nyema amesema uwepo wa  madaktari bingwa na bobezi hao utasaidia kupunguza msululu wa wagonjwa waliokuwa wanahitaji huduma za kibingwa, lakini walikuwa hawazipati kwa wakatika kutokana na upungufu wa madaktari hao katika hospitali za rufaa.

Dk Nyema amesema wana kila sababu ya kuishukuru Wizara ya Afya kwa kufikisha huduma za kibingwa kwa sababu itasaidia kupunguza changamoto ya matibabu kwa magonjwa mbalimbali.

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Afya, Getrude Naphtal amesema kambi hiyo ilizinduliwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu Mei 6, mwaka huu mkoani Iringa.

Amesema huduma za kibingwa zitatolewa kwenye kanda nane katika hospitali za wilaya 184 nchini na  kila wilaya itafikiwa na madaktari bingwa na bobezi watano.

Mkazi wa Jijini Mbeya,Ester Damian amesema  huduma hizo ni  mkombozi mkubwa kwa wananchi wa kipato duni ambao wanakosa huduma kutokana na kukosa fedha.